MADHARA YA KUPIGA RAMLI/BAO. - waleo blog

Breaking

Wednesday 1 April 2020

MADHARA YA KUPIGA RAMLI/BAO.


#ELIMIKA

Ramli/bao ni kitendo cha kupandisha majini kichwani(pepo),kuchora   michoro fulani fulani ima chini ya arthini ama karatasini kwa lengo la kugundua majambo yaliyofichikana na yajayo.Mambo haya hufanywa  na waganga wa kishirikina(wachawi).

Kwa  wale waishio kupitia  mapokeo ya dini kuu mbili duniani yaani Uislamu na Ukristo majibu kuhusu  ramli ni kama ifuatavyo.
BIBILIA INASEMAJE.
Hali ya kupiga ramli imekatazwa na Mungu. Imeandikwa katika Kumbukumbu la torati 18:9-13 "Utakapo kwisha ingia katika nchi akupayo Bwana  Mungu wako, usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale na asionekane mtu yeyote ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao wala mtu atazamaye nyakati mbaya wala mwenye kubashiri wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo wala mtu apandishaye pepo wala mchawi wala mtu aombaye wafu kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo, Bwana Mungu wako anawafukuza mbele yako."
Mungu ndiye ajuaye mambo yajayo. Imeandikwa, Isaya 8:19 "Na wakati watakapokuambia tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi walio na ndege na kunong, ona je! haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? Je waende kwa watu walio kufa kwa ajili ya watu walio hai?."


UISLAMU UNASEMAJE NAO.
Aina zote za hawa watu ni sawa ikiwa ni mtabiri wa nyota, kusoma viganja au kupiga ramli na zote hizi  zimekatazwa.Mwenyezi Mungu Anasema:
“Enyi Mlioamini! Bila shaka ulevi, na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga ramli ni uchafu katika kazi za shetani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate kufanikiwa” (5: 90).
Na Mtume Muhammad (S.a.w) amekataza jambo hilo, hivyo inatakiwa tujiweke kando kabisa.
Mambo yote haya ni haramu na yeyote mwenye kuamini kuwa jambo fulani limetokea kwa sababu ya nyota kadhaa na kadhaa amemkanusha Allaah kama Alivyosema katika hadithi ifuatayo:
(Yeyote atakaye jimai (kufanya kitendo cha ndoa) na mwanamke mwenye hedhi, au kwa kutumia njia ya nyuma(kulawiti), au kumkaribia mtabiri na kuamini aliyoambiwa, basi amekufuru yale aliyoteremshiwa Muhammad).
 [Hadithi Sahihi, imesimuliwa na Mus-habu-Sunnan na wengineo]
Na kufanya hivyo ni kuingia katika elimu ya ghaybu (mambo yaliyofichika ya Allaah) ambayo hakuna aijuwae ila Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) na humpeleka mtu kuingia katika shirki.  Na Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) humghufuria mtu dhambi zote ila shirki kama Alivyosema:
"Hakika Mwenyezi Mungu hasamehi kushirikishwa, na husamehe yaliyo duni ya hilo kwa amtakaye. Na anayemshirikisha Mwenyezi Mungu basi hakika amezua dhambi kubwa"
[An-Nisaa: 48

Nasaha zetu ni kuwa tumuamini Allaah na nguzo zilizobakia za Imani kama Qadar, hivyi tutaondokana na matatizo ya kumkufuru Allaah kwa kwenda kuangaliliwa na hawa wapiga bao, ramli na wengineo.

Hiyo ndio ramli na makatazo yake, pande kuu mbili za dini zenye wafuasi wengi duniani.
Usikae mbali nasi zingine zafuata……..
 Usisite kwa maoni na lolote lile lihusulo sisi na tukifanyacho.
                                                            +255767611645
                                                           +255715080716
                                                            adamgome96@gmail.com
                                                            Mwanaharakati1992@gmail.com


No comments:

Post a Comment

Pages