MUZIKI NCHINI TANZANIA.. Mwendelezo. - waleo blog

Breaking

Wednesday 1 April 2020

MUZIKI NCHINI TANZANIA.. Mwendelezo.


Mwendelezo wa makala iliyopita

Kiufupi, wakati huu ushindani ulikuwa mkubwa sana na wanamuziki au waimbaji wengi walihama kutoka bendi moja kwenda nyingine hasa kwa kufuatia utitiri wa mabendi ya muziki wa dansi nchini. Kipindi hiki ndicho alichokuja mkali wa sauti nchini Tanzania King of Melody (Christian Bella) akitokea nchini jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Kipindi hiki ndicho kilichounda bendi ya Wajelajela Original (Stono Musical), baadaye FM Academia chini ya ungozi wake Nyoshi El Sadat. Hii FM Academy ilikuwa moja na Stono Musica kabla ya kutengana na Nyoshi akabaki na jina halisi lakini kaongeza neno kama "The Dream Team". Zama hizi wanamuziki vijana wa kikongo walifurika hasa kuja nchini Tanzania.
Kwa upande wa muziki wa kizazi kipya, ukiacha wale walioanza kabla ya 2000, hapa anakuja Dully SykesManzese CrewWandava Creek, Wehu Kumi Ngangari (W TEN N), TIDJay MoeNgwairDaz NundazMadeeMandojo na Domo KayaMr. BlueComplexDudu BayaJuma Nature na FSGA.Y.G.K.Q ChillahMwanaFALady Jay Dee na Ray C. Jay Dee ndiye msanii wa kwanza kurekodi albamu yenye gharama kubwa mno kuliko zote tangu kuanza kwa muziki wa kizazi kipya. Kwa kipindi kile cha mwanzoni mwa miaka ya 2000,ndiye aliyeanza kupiga video na Benchmark Production kwa kipindi haikuwa rahisi sana kufanya kazi na kampuni hiyo. Jay Dee na A.Y. ni wasanii wa mwanzo kabisa kuthubutu kutoka nje ya mipaka ya Tanzania katika kufanya muziki na wasanii wa nchi za nje.
Hili halijawahi kufanywa hapo awali na wasaniii wowote wa kizazi kipya isipokuwa wawili hawa. Ray C, ni moja kati ya wasanii wa Bongo flava walioweza kufanya vizuri, lakini nae anasa za maisha zilimfanya kufuta urithi wake wote katika muziki. Haonekani tena thamani yake hasa kwa kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya. Kulikuwa na makundi yaliyoingia na kutoka. Aidha kwa kukosa udhamini au kujitangaza vya kutosha. Kundi kama Boyz from the Army, Born Crew, Hot Grils, Big Dog Pose (BDP), Hot Port Family, Wateule, Mambo Poa, Uswahilini Matola, na wengine wengi waliingia na muda mchache hawajafua dafu wakapotea jumla. Sehemu ya kikosi cha wanamuziki waliokuwa wanajiita New Jack Family, watoto wa Kariakoo. Nao walizingua sana katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya. Hasa kwa msanii wao Dully Sykes. Kundi kama G.W.M. baadaye likaja kuwa sehemu ya Wachuja Nafaka huku kukiwa na ongezeko la Juma Nature na Doro.
Wachuja Nafaka lilikuwa kundi la mradi tu (super group) lililodumu muda mchache tu. Wasanii wengine waliotamba katika 2001/2002/2003/2004 ni pamoja Zahrani a.k.a Big Punisher wa Bongo, Spulla, Bushoke, Mr. Nice ambaye kiukweli alitamba kupita maelezo na nyimbo za kuchukua hala za kitoto na kuzirudia katika mtindo wa Bongo Flava aliotamba nao kwa jina la TAKEU.Aliupeleka muziki wa kitanzania mbali sana, hasa katika nchi za BurundiRwanda, Kongo na nchi zingine za Afrika.Ubaya ulioje!? hakudumu sana, hasa kwa kuendekeza anasa za maisha na kuepelekea kuanguka mazima katika fani ya muziki. Buibui, Mpaki, Nurueli, Bab Lee, Snoop Lee, Man X na wengine wengi.
Professor Jay katika upande wa wasanii wa kiume, alionekana kuunyanyasa sana muziki wa kizazi kipya katika miaka ya 2001­­-2005. Zama hizi Professor Jay alionekana kutokuwa na mpinzani, inasemekana yeye ndiye aliyesababisha wazee wasikilize muziki wa kizazi kipya. Ilikuwa mwaka 2000 na kibao chao cha Chemsha Bongo ambamo maneno mazito aliyoongea humo yalipelekea wazee wengi kusikiliza muziki huu. Kabla ya 2000, wazee wengi waliona muziki wa kizazi kipya ni kama uhuni tu. Huenda Professor Jay ndiye aliyevutia vijana wengi kuingia katika muziki kama jinsi ilivyo kwa siasa, Zitto Kabwe kuvutia vijana wengi kujiunga na siasa.
Huwezi kutaja muziki wa kizazi kipya bila Prof. Jay. Mb Doggy ndiye mwanzilishi wa muziki wa mapenzi mazito, hata kama awali waliimba, lakini si kwa kiwango cha Mb Doggy. Mwaka 2005-2006 ilikuwa ni kipindi chake cha kuunyanyasa muziki wa kizazi kipya. Mb Doggy kutoka Tip Top Connection alionesha uwezo wake mkubwa sana katika tasnia hii. Miaka hii ya 2005-2006 Ferouz nae alikuja juu sana. Lakini hakwenda mbali.
Ni miaka hii, alipokuja Matonya, Abby Skills, Enika, Ali Kiba, Queen Darleen ijapokuwa alikuwepo tangu enzi za historia ya Kweli ya Dully Sykes, lakini hakuwa msanii kama msanii mpaka kipindi hiki. Kipindi hiki muziki wa taarab ulipamba moto. Mwaka wa 2006, Jahazi Modern Taarab ilianzishwa chini ya uongozi wake Mzee Yusuph. Mzee Yusuph aliufikisha mbali sana muziki huo, alisababisha kila mtu asikilize taarab hasa kwa tungo zake. Baadaye zikazuka bendi nyingine nyingi tu za taarab.
Katika miaka ya 2010.
Katika kipindi hiki, muziki wa kizazi kipya na muziki wa dansi ulibadilka sana. Vijana wengi walikuja katika muziki wa dansi. Lakini Bongo flava imepiga hatua maradufu. Msanii kama Diamond Platnumz ameupeleka mbali muziki wa Tanzania nje ya nchi kwa kiasi kikubwa kupita msanii yeyote yule tangu muziki huu ulipoanza. Katika kipindi hiki, rundo la wasaniii wa muziki wa Bongo flava walibatizwa kama wabana pua, waliongezeka na kuigana kupita kiasi. Watayarishaji wa muziki huu waliongeza maradufu. Bongo flava, ilianza kuchukua miundo mbalimbali ya miziki mingine kama vile Kwaito, Zouk Rhumba, Singeli, Raggae, muziki wa Nigeria hasa waliiga na kadhalika. Na ndicho kipindi kilichoanza na ushamba katika muziki, hasa kwa kuanzisha makundi maarufu kama team kati ya msanii na msanii.
Lakini timu zilizokuwa na ushandani mkubwa ni za Ali Kiba na Diamond. Kipindi hiki ndicho walichovuma akina Ben Pol, Top C., Bob Junior, DarassaOne IncredibleNikki MbishiNikki wa PiliGeez MabovuBaraka da PrinceGalatone TenaSamirBelle 9Kassim MgangaNuh MziwandaZ. AnthonyDullayoSam wa KweliBarnabaMarlawIzzo BusinessMabesteLinahGosbyGodzilla na wengine wengi tuWCB lebo ya muziki iliyozalisha wasanii wapya kama Harmonize, Rayvanny. Vile imechukua wasanii wengine maarufu kama Richie Mavoko. Kwa pamoja wameweza kuutingisha muziki wa kizazi kipya kwa mwaka wa 2015/2016. Vilevile kuanzia Agosti 2015, Darassa ameonekana kuutawala muziki wa kizazi kipya kwa kiasi kikubwa sana. Hasa kufuatia yeye anafanya hip-hop. Huenda Darassa ni msanii pekee wa hip-hop aliyeweza kufikisha watazamaji wengi kwa muda mfupi katika Youtube kuliko msanii yeyote yule wa hip-hop wa kitanzania hasa kwa kufuatia kibao chake cha Maisha na Muziki na Too Much kilichotoka Julai 15 na Muziki Novemba 23, 2016. Vilevile kipindi hiki ndicho kulipozaliwa muziki wa Singeli. Wanamuziki maarufu wa Singeli ni pamoja na Man FongoMsaga SumuSholo Mwamba na wengine wengi.

Haya bwana, huo ndio muziki wa Tanzania na asili ya muziki kiujumla
Sambaza kwa wengine waujue/wakumbuke.
Maoni,ushauri hapa.
                 0767611645
                 Mwanaharakati1992@gmail.com
                 adamgome96@gmail.com
                 +255715080716

No comments:

Post a Comment

Pages