MJUE KIFARU NA MAADUI ZAKE ,KISHA JIEPUSHE - waleo blog

Breaking

Saturday 21 December 2019

MJUE KIFARU NA MAADUI ZAKE ,KISHA JIEPUSHE


#UTALII        
  Kifaru ni mnyama mwenye nguvu na aliyejengeka na kupambika na pembe moja (1) kubwa iliyo gawanyika katika pacha mbili (2) usoni  mwake.Kuna aina mbili za kifaru, ambazo ni Kifaru mweupe na Kifaru mweusi.
           Maeneo anakopatikana huyo Kifaru mweupe ni katika nchi ya Uganda na nchi ya Afrika ya kusini(South Africa)/au rasi ya tumaini jema.Kifaru mweusi nae anapatikana katika nchi ya Tanzania mkoa wa  Arusha mbuga ya Serengeti ,  Ngorongoro  na pia nchini Kenya.
           Uhai wake.  Wataalamu wa wanyama pori waliweza kumchunguza  mnyama huyu kifaru na kubaini kuwa, kifaru anauwezo wa kuishi ndani ya miaka 40—50 kutokana na mazingira anayoyapitia.
            Kifaru  anashika ujauzito ndani ya miezi 15—18, na dume la kifaru ni kubwa kuliko jike.Chakula kikuu cha kifaru ni majani na hula chakula hicho nyakati za asubuhi na jioni.
            Kifaru  aliyekamilika katika ukubwa wake ana kilo 1000-1500.Lakini pia Kifaru ni moja  kati ya wanyama watano[5] wakali duniani, yaani (big five) hapa tunamaanisha uwepo wa Tembo, Simba, Chui na Nyati.
             Ulinzi na upambanaji, Kifaru  hutumia pembe yake  kupambana na  Simba pindi anapotaka  kuwadhuru watotowe, na wakati mwingine hutumia kupigana wao kwa wao.Kifaru hutumia  mkia wake kuukojolea na kumwagia binadamu pindi atakapo panda juu ya mti, palee alipo taka kumfanyia uhalifu.
             Adui mkubwa,  tena mkubwa asiye na haya wala huruma kwa mnyama Kifaru ni,  mimi mwandishi wa makala  na msomaji wa makala hii(binadamu) na wakati mwingine Simba huwinda watoto wa Kifaru.
            ‘’ Hakika mkamilifu ni mungu pekee kama vile yesu alivyosema ndani ya  Bibilia,’’Hakuna aliyemkamilifu yule ambaye ametoka katika tumbo la mama yake’’.   Swali la mwandishi kwenu. Tumemkosea nini Kifaru mpaka sisi binadamu ndio tunakuwa adui yake mkuu?.Tuacheni tabia hii’’.

Huyu ndiye kifaru kwa uchache..

Usisahau kufolo,maoni na ushauri  katika makala na habari mbali mbali
   Kwa huduma ya utalii, usisahau kututazama hapa,
   Malamboaziz14@gmail.com/0717475992/0782080716     

No comments:

Post a Comment

Pages