MLIO WA BUNDI SI, UCHURO. - waleo blog

Breaking

Wednesday 25 March 2020

MLIO WA BUNDI SI, UCHURO.


#Utalii

Bundi  ni ndege mbuai wa familia Tytonidae na jenasi mbalimbali ya familia Strigidae. Leo tutaitazama familia ya Strigidae.Kizazi hiki kinaainishwa katika nusu familia na jenasi moja ya nusu familia Striginae.
Bundi hawa wana kichwa kikubwa chenye umbo la mviringomkia mfupi na rangi ya kamafleji. Kwa kawaida jike ni mkubwa kuliko dume. Mabawa yao ni marefu na mapana. Hula ndege na wanyama wadogo wadogo,hasa wagugunaji. lakini watambaaji na wadudu wakubwa pia. Jike huyataga mayai 2-7 katika tundu la mti au tago lililoachwa na ndege mwingine na pengine katika sanduku la kutagia.
Bundi wengi huwinda usiku na hupumzika mchana. Manyoya ya uso yapeleka mawimbi sauti kwa vipenyo vya masikio ambavyo kimoja kipo juu kidogo kuliko kingine. Hivyo wanaweza kumkamata mbuawa bila kumwona. Mbuawa hawezi kumsikia bundi akija, kwa sababu mabawa ya bundi hayafanyi sauti yo yote kwa kuwa kingo ya mbele ya manyoya ya mabawa yamekerezeka kerezeka na lile ya nyuma lina matamvua. Hii inapunguza vurugu ya hewa na kwa uvumi.

Bundi ni oda ya ndege wala nyama wanaowinda saa za usiku hasa wakati wa giza.
Ndani yake kuna familia mbili:
·         familia ya Strigidae
·         familia ya Tytonidae
Baadhi ya jamii chache zimekuwa zikihusisha bundi na ushirikina ama uchawi, hivyo kutia wengi mashaka, hasa wanaposikia sauti ya ndege huyo nyakati za usiku.
 Usiogope wala kuhuzunika pindipo usikiapo mlio wa bundi usiku,bali yakupasa kufahamu ya kuwa ni hali yake ya kawaida kama ilivyo kwa wanyama wengine wakiwa wanatoa mlio,mfano mbuzi,ng’ombe n.k.Utofauti wa bundi ni kulia usiku na mapokeo ambayo tuliyapokea kwa babu zetu kuwa ni uchuro.


Usomapo makala hii,ninaamini utakuwa mwalimu kwa wengine wa kuwaondoa hofu..

Usisite kutunasihi pale tutelezapo, kwa maana mkamilifu ni MUngu pekee..
Ushauri na maoni,,,,
+255767611645
+255715080716
Adamgome96@gmail.com



No comments:

Post a Comment

Pages