DADA/KAKA,MKE/MUME BORA HUYU HAPA - waleo blog

Breaking

Wednesday 19 February 2020

DADA/KAKA,MKE/MUME BORA HUYU HAPA


#MAHUSIANO 
  

       Wahenga wanasema, kosea njia utaelekezwa kwa kupita,mtoto hupotea lakini mkubwa huchelewa kufika….Oyo,,usikosee kumpata mume ama mke mwema utajuta kuzaliwa.Katika makala hii leo nimeona tukumbushane ama kufahamishana katika zile sifa za mume ama mke anepasa kuolewa na kukuoa.Zifuatazo zitakusaidia kumchagua mwenzi wako.

1.  Mwanamke/mume kuwa na dini, tabia na maadili mema. Dini si ya kinadharia bali imfanye abadilike katika mambo yake yote kama kuwa na tabia njema na maadili mema.Hii ni kwa waaminio kuhusu dini zilizokuja na wageni,ndio sababu yetu waafrika kuwa wastaarabu.

2.  Kumpendeza mume/mke anapomuangalia. Kupendeza na uzuri ni vitu ambavyo kila mwanamme ana kile anachokiona kuwa ni kizuri. Hivyo hapa wanaume wazingatie sana kwenye kuangalia kitu ambacho kitampendeza amwangaliapo mkewe,mfano rangi (mweupe ama mweus)i,mnene ama mwembamba,mwenye matiti madogo ama makubwa ama mwenye makalio madogo ama makubwa.Hivi ni kwa uchache zaidi.

3.  Kuwa ni mwenye kuingiliana na watu na mwenye moyo wa bashasha kabisa. Mafungano ni baina ya familia mbili, yako na yake. Kwa ajili hiyo anatakiwa awe ni mwanamke mwenye kufanya mahusiano na watu wako wa karibu ili kuwe na maendeleo na uhusiano mwema.

4.  Mwenye kuzaa/kupanda mbegu bora, na hili kama wataalam walivyosema, ni kuangalia kizazi cha madada zake na jamaa zake wa karibu.Na ikatokezea mumgu hakumjaalia kizazi, basi turejee katika dini zetu zinasemaje.


Hata hivyo, muhimu zaidi ni dini na ikiwa ana sifa nyingine ziwe ni baada ya hiyo sifa ya kwanza.Unaweza kuhoji kwa nini dini? Watu tuliowengi barani Afrika,Asia na sasa mpaka ulaya tunaamini ya kuwa kama si kuja kwa dini zilizo mtangaza Mungu asiyeonekana (dhahania)basi ustaarabu tulio nao hivi leo  tusingekuwa nao.Mfano, zamani  hizo kabla ya hizi dini watu waliamini ya kuwa mototo mlemavu ni laana na hapaswi kuishi isipokuwa auwawe.Zilipokuja dini zikatuelimisha ya kuwa watu wote wanahaki ya kuishi bila kujali ulemavu wao.Hivyo basi tunaposema kigezo kikubwa cha mume ama mke ni dini kwa sababu za msingi zifuatazo.Ndani ya hizi dini yapo mafundisho ambayo yanamtaka mtu asiwe mshirikina,asiwe mwenye kuchezea mali kwa fujo,awe mwenye kuwaheshimu wakubwa kwa wadogo na chochote utakachokifikiria katika akili yako basi katika dini zetu hizi majibu yapo.”Ila ni nani utamuuliza  kazi ni kwako”.kwa mantiki hiyo, mwanamke au mwanaume kama atakuwa ameshiba katika mafunzo ya dini ni wazi ya kwamba ndoa hiyo ni ya kudumu tukiachana na makosa ya kibinadamu.mfano mboga kuzidi chumvi ama mume wangu anifikishi.

           Share na wenzako wapate  mke ama mume  mwema na sio bora niolewe/kuoa.

No comments:

Post a Comment

Pages