USISEME HAYA UKIACHWA,KUBALI UMEACHWA. - waleo blog

Breaking

Thursday 23 January 2020

USISEME HAYA UKIACHWA,KUBALI UMEACHWA.


 #Mahusiano

Habari ya muda huu ndugu wasomaji wetu, karibuni tena tujadiliane mambo mbalimbali unayopaswa kuzingatia pindi unapoachwa na mpenzi wako .

1: Usiharakishe uhusiano mpya.
Unapoachana na mpenzi wako basi jipe muda kutafakari mapungufu yako na wapi ulikuwa unakosea.
Kuanzisha uhusiano mpya baada ya kuachwa huwa mara nyingi unaenda sehemu ambayo sio sahihi na utajiku unaambulia kuachwa.
Utahitaji mtu wa kukufariji na yeye akatumia mwanya kukupa care as if he/ she is into you.. but hakuna kitu kama hicho mtachokana mapema na kusiwepo na mapenzi ukabaki unatanga tanga na usipokuwa makini basi utatumika sana.

2. Usiseme hauta penda tena.
Kosa la mtu mmoja basi usijumuishe kwamba watu wote watakuwa kama mpenzi wako, ikakusababisha kutokupenda watu wanatofautiana.
Haina maana aliyekuumiza kila mtu ataku cheat au kwasababu mpenzi wako alikuwa anakutukana na kukupga ukahisi basi wote wapo hivyo.
Ni vizuri ukamsoma mtu tabia zake kabla hujajiingiza kwenye uhusiano. Anza kutengeneza muelekeo wa penzi unalotaka.


3. Acha upweke jichanganye na watu.
Watu wengi wakiachika basi wanajisahau na kuanza kuomboleza na kuacha kufanya mambo ya msingi.
Ukiomboleza uhusiano wako uliopita mama/baba hapo utakuwa hujaacha wala kuachika.
Changamka jichanganye na watu na ufurahi, hii itapelekea kusahau mapema na kufanya mambo ya maendeleo.
Haitakiwi wewe kuwa mnyonge wakati ulie achana naye anaruka majoka anafurahi maisha na mambo yake yanaenda.
Nataka nikueleze, maisha ni mafupi achana na kufikiria kuachwa na mpenzi wako. Unatakiwa kujua kuna maisha baada ya kuachwa.

4. Ukiachwa kubali.
Usimgande mtu asiye kupenda na misamaha isiyokuwa na tija.. kama alikuacha inamaana anasababu nyingi za kukuacha.
Ukishaona katika uhusiano wako mtu kosa dogo anakimbilia kutoa maneno ya kuachana ujue hakupendi bali anakutumia tu kimwili.
So akikuacha achika, usimtafute wala nini wala hakuna mambo ya tubaki kuwa marafiki na blah blah .. kama kachoka kuwa mpenzi wako ambae mna share vitu vingi zaid ya urafik ataweza kuwa rafiki huko ni kupotezeana muda na kuchoshana.

5. Acha mambo ya kukumbushia ni ujinga uliopitiliza.
Kama mliachana mkiwa wapenzi na kila mmoja akaenda njia yake.. mnakumbushia nini!?? Akili zenu zinawaza nini? Mnajua kama kuna magonjwa!?? atabak kuwa mpenzi tu aliyeachwa  na unatakiwa kwenda mbele usikubali kurudi nyuma.
Suala la kuanza kukuambia mkutane na kuanza kukumbushiana huku ni sawa hamjaachana ila mnaendekeza umalaya.
Usiwe tegemezi kwenye mahusiano yako kwani kuachwa umeanza wewe mpaka ushindwe kuendesha maisha yako.
Hakuna jambo ambalo unadharaulika kama kuachwa halafu unaanza kumng’ang’ania mtu ambaye hana muda na wewe.



Hebu tubadilike jamani kuna maisha baada ya kuachwa acha kuumiza akili kisa umeachwa.
Share,like,comment na usisahau kutufuatilia.


No comments:

Post a Comment

Pages