WAZIRI MKUU ATANGAZA WANAWAKE KUPANDA MABASI BURE - waleo blog

Breaking

Tuesday 4 June 2019

WAZIRI MKUU ATANGAZA WANAWAKE KUPANDA MABASI BURE


Waziri Mkuu atangaza wanawake kuanza kupanda mabasi bure


Waziri Mkuu wa jimbo la Dheli nchini India, Arvind Kejriwal siku ya jana alitangaza usafiri wa bure kwa wanawake wote wanaosafiri kwa kutumia mabasi na treni za serikali.

Hatua hiyo inakuja baada ya visa vya kina mama kunajisiwa ndani ya magari ya kibinafsi kuongezeka. Waziri Mkuu alisisitiza kuwa usafiri wa umma ndio salama zaidi kwa wanawake wote.

Serikali ya India itatumia dola za Marekani Milioni 172 kila mwaka kulipa nauli za wanawake hao, hata hivyo hatua hiyo imeonekana kuwa ya kisiasa, kwa kuwa jimbo hilo linajitayarisha kupiga kura mwaka ujao.

No comments:

Post a Comment

Pages