KLABU IPI ENGLAND KUMNG'OA SAMATTA GENK? - waleo blog

Breaking

Thursday 6 June 2019

KLABU IPI ENGLAND KUMNG'OA SAMATTA GENK?




Klabu nyengine za England ambazo zinamuwania Samatta ni Aston Villa, Watford, Leicester na Burnley.
Kwa mujibu wa gazeti la The Sun la Uingereza Samatta ana thamani ya Pauni milioni 12.

Samatta ambaye bado ana mwaka mmoja kwenye mkataba wake na mabingwa wa Ubelgiji KRC Genk pia amezivutia klabu za Roma ya Italia na Lyon ya Ufaransa.

Mshambuliaji huyo ambaye aliongoza kwa kupachika mabao msimu uliopita nchini Ubelgiji ameweka wazi kuwa anataka kuelekea nchini England msimu ujao.

"Kwa sasa hivi siwezi kusema sana, ni kitu ambacho kipo kwenye mchakato nasubiria kitakapokuwa tayari na wakati utakapofika nitaweza kukizungumza. Lakini sijioni tena Genk, namuomba Mwenyezi Mungu litimie, lakini ikishindikana bado nina mkataba na Genk," aliiambia  Azam TV.

Klabu ya Brighton imekuwa ikimfuatilia Samatta kwa muda mrefu na kocha wa timu hiyo kwa msimu uliopita Chris Hughton alikuwa akivutiwa sana na mchezaji huyo.

Kocha mpya wa klabu hiyo Graham Potter pia anavutiwa na uwezo wa Samatta.

Samatta ni nahodha wa Tanzania kwa sasa yupo kambini na timu ya Taifa Stars wakijiandaa na michuano ya bara la Africa (Afcon 2019) yatakayofanyika nchini Misri mwezi huu.



FOLLOW,COMMENT,SHARE USIPITWE NA HABARI MPYA

No comments:

Post a Comment

Pages