ZITAMBUE HIFADHI ZETU/MIKUMI NATIONAL PARK - waleo blog

Breaking

Sunday 16 June 2019

ZITAMBUE HIFADHI ZETU/MIKUMI NATIONAL PARK


 #UTALII
                                    

            Hifadhi ya taifa Mikumi ipo katika nchi ya Tanzania, mkoa wa Morogoro, wilaya ya Kilosa,  mamlaka  ya mji mdogo wa Mikumi.Mbuga hii ya Mikumi  imeanziswa  mwaka  1964.Neno Mikumi  limetokana  na  miti mingi aina ya  Mikoche /Mkumbi [ Mikumbi]   kwa  wingi,ambayo  ilikuwa  mingi  sana  eneo  husika.Kauli  mbali mbali zilisemekana kwamba  kutokea kwa neno  mikumi  ni matokeo  ya mzungu  kushindwa kutamka neno  Mkumbi na  kusema  Mkumi, na tangu hapo  ndipo  ikawa  sababu  ya kutokea  kwa  neno Mikumi.Mbuga  hii ya  ya mikumi ina  kilometa  za mraba  3,,230 sq na ni hifadhi  ya  tano{ 5} kwa  ukubwa nchini   Tanzania, na ya kwanza ni  hifadhi ya Ruaha  ya pili Serengeti, Katavi na Mkomazi.
        Katika hifadhi ya taifa mikumi kuna miti mbali mbali ya asili, ndege na wanyama.Katika wanyama wanaojulikana  kama big five yaani  Kifaru,Tembo,Simba,Chui na Nyati. Katika  hao big  five hifadhi ya mikumi wapo  wanne {4} tu yaani  big four, ambao ni Tembo, Chui,Simba na Nyati.


 TEMBO
      Tembo  ndio mnyama mkubwa duniani.Tembo  wapo wa aina mbili   duniani ,yaani  {a}  African  Elephant (b) Asian Elephant. Tanzania anapatikana  wa aina moja tu ambaye ni African Elephant..Tembo anaishi miaka 60-70  na Tembo mkubwa ana kilo 6000 dume na jike kilo 4000.Lakini pia  Tembo anashika ujauzito  miezi  22  hadi  miaka 2  na  mtoto wake akimzaa anakuwa na kilo  120  hadi  150..
         Tembo  mkubwa kwa siku anakula  majani kilo zisizo pungua 150-300.Tembo pia  katika masaa  ishirini na nne [24] ya kila siku, anatumia  masaa  18  kula chakula usiku na mchana..
         Tembo  husumbuliwa na maadui zake  wakuu  2.Ambao ni  binadamu na pia  magonjwa..
INAENDELEA

#USISAHAU KUFUATA(FOLLOW  ) BLOG YETU KWA HABARI NA MAKALA  MBALI MBALI.
Kwa  maswali binafsi kuhusu wanyama na  shughuli za  utalii
Piga simu no  0717475992/0782080716.

No comments:

Post a Comment

Pages