DR. KIGWANGALA AITAKA BODI YA UTALII KUWEKEZA KATIKA MAWASILIANO YA KISASA - waleo blog

Breaking

Thursday 6 June 2019

DR. KIGWANGALA AITAKA BODI YA UTALII KUWEKEZA KATIKA MAWASILIANO YA KISASA

 
           


              

Waziri wa maliasili na utalii, Dk Hamisi Kigwangalla ameitaka bodi ya utalii Tanzania (TTB) kuwekeza zaidi katika matumizi ya njia za kisasa za mawasiliano na mbinu rahisi zenye gharama nafuu katika kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Aliyasema hayo Dodoma wakati akizindua rasmi bodi hiyo ambayo Aprili, mwaka huu, Rais John Magufuli aliiongezea muda wa miaka mitatu.

Waziri Kigwangalla alisema kiu yake ni kuona sekta ya utalii inakua na kuchangia pato la taifa, hivyo aliieleza bodi hiyo kuwa ina wajibu wa kuendelea kubuni na kuongeza mbinu mpya za kutangaza utalii ili kuleta tija.

Alisema bodi hiyo inaweza kufanikiwa zaidi kama itafanya kazi pamoja na wadau na taasisi nyingine za wizara ili kuongeza idadi ya watalii wanaoitembelea Tanzania.

Aliweka msisitizo katika matumizi ya mifumo ya kisasa ya mawasiliano ili kupanua wigo wa kutangaza vivutio vya utalii kuliko ilivyo sasa.

Dk Kigwangalla aliipongeza bodi hiyo kwa kuendelea kuhamasisha utalii nchini kwa kuja na kaulimbiu ya Tanzania Unforgettable ambayo imekuwa chachu kwa taifa hasa katika kuitangaza sekta hiyo Kitaifa na Kimataifa.

"Mnatakiwa kuwa na mkakati mahususi wa kukamata masoko mapya ya watalii kutoka nje ya nchi kwa kufanya matangazo angalau mara tatu kwa mwaka, ili kuvutia watalii wengi zaidi,"alisema.

Alizitaja nchi ambazo bodi inatakiwa kuweka mikakati mahususi kuwa ni Marekani, Hispania, Urusi na nchi za Falme za Kiarabu zikiwemo za Dubai na Oman ambazo watu wake wakiwemo wasomi, wafanyabiashara, wanamichezo na walio maarufu wanapenda kwenda kupumzika kwa muda mrefu na kutumia fedha nyingi kwa utalii.



No comments:

Post a Comment

Pages