UPANA WA ELIMU.. Inaendelea - waleo blog

Breaking

Wednesday 1 April 2020

UPANA WA ELIMU.. Inaendelea


Inatoka ukurasa uliopita(mwendelezo)

Mitaala
Somo la taaluma ni tawi la elimu ambalo hufunzwa rasmi katika vyuo vikuu ama kupitia njia zingine kama hizo. Kwa kawaida, kila somo huwa na masomo mengine ama matawi na mipaka ya kuyabainisha mara nyingi huwa si dhahiri na na mara nyingine husababisha utata. Mifano ya masomo ya kitaaluma yenye upana ni kama vile sayansi asilia, hesabu, sayansi ya komputa, sayansi za jamii, sayansi za binadamu na sayansi za matumizi.
Kwa wakati huu, kugawika kwa elimu katika mitindo tofautitofauti hukubalika na wengi. Huenda ikawa kuwa mitindo  ya kujifunza ndiyo ya kawaida.
·         Kuona: Masomo yenye misingi ya kutazama kwa makini na kuona kile kinachosomwa.
·         Kusikiza: Kusoma kwa misingi ya kusikiliza maelezo/habari.
·         Masomo husishi: Kusoma kwa misingi ya kutumia mikono na vitendo husishi.
Imedaiwa kuwa kulingana na mtindo wa kujifunza unaopendelewa kwa mbinu tofautitofauti za kufunza huwa na matokeo ya viwango tofauti. Umuhimu wa nadharia hii ni kuwa kunakofaa na inapaswa kutumia mbinu mbalimbali za kufunza zinazojumlisha mitindo yote mitatu ya kufunza ili wanafunzi tofautitofauti wapate fursa ya kujifunza kwa njia inayowafaa. 
Kujifunza
Kujifunza ni kutaka kujua juu ya jambo fulani ambalo hukulijua kabla. Hata jambo zuri kuhusu kujifunza ni kwamba hakuna mtu yeyote mwenye uwezo wa kukiweka mbali nawe kitu hicho ambacho umejifunza.
Walimu wanapaswa kuelewa somo vilivyo ili kuwasilisha umuhimu wake kwa wanafunzi. Shabaha hapa ni kuunda misingi ya ujuzi kamili ambayo wanafunzi wanaweza kutumia kujijenga zaidi kwani wamewekwa wazi kwa matukio mbalimbali ya maisha. Walimu wazuri huweza kutafsiri habari kama hukadiria vizuri, hutumia mazoea na hekima hadi kwa elimu husika ambayo mwanafunzi anaweza kuelewa, kuhifadhi na kupititishia wengine.
Utafiti kutoka Marekani unatoa maoni kuwa ubora wa walimu ndio kigezo kinachoathiri mafanikio ya wanafunzi, na kuwa nchi zinazopata alama za juu katika mtihani au majaribio ya kimataifa zimeweka sera chungu nzima zinazohakikisha kuwa walimu wanaoajiriwa ndio bora. 

Teknolojia ni kigezo muhimu katika elimu. Tarakilishi/kompyuta na  rununu yaani simu za mkononi zinatumiwa katika nchi zilizoendelea kuimarisha elimu iliyothibitishwa na kukuza njia mpya za elimu kama vile elimu ya mtandao (masomo ya mbali). Wanafunzi hupata fursa ya kuchagua wanachotaka kusoma.
Kuenea kwa tarakilishi pia kunamaanisha kuongezeka kwa programu za kompyuta na kuongeza habari mtandaoni. Teknolojia hutoa vifaa muhimu vinavohitaji ujuzi mpya na uelewa wa wanafunzi zikiwemo njia nyingi za mawasiliano, na huleta njia mpya za kuhusisha wanafunzi kama vile mazingira ya kujifunza.
Teknolojia inatumiwa si tu katika wajibu wa kutawala katika elimu bali pia katika kuwaelekeza wanafunzi. Matumizi ya teknolojia kama vile virusha maandishi (power point) na ubao mweupe hutumiwa kunasa akili za wanafunzi darasani. Teknolojia vilevile hutumiwa kuwatahini wanafunzi. Mfano mzuri ni mfumo wa kuvutia hadhira (ARS),ambao huruhusu majibu ya mitihani moja kwa moja pamoja na majadiliano darasani.
Teknolojia pia imekuwa mojawapo wa maktaba katika elimu ambamo vitabu, ripoti za utafiti, n.k. huchapishwa. Tovuti zinazochapishwa vitabu, ripoti na tansifu zimekuwa na manufaa kwa wasomi. Zinawapa uwezo wa kupata vitabu maalum kwa ujumbe fulani tofauti na maktaba za kizama ambazo humlazimu mtu kusoma kwa urefu na upana kupata ule ujumbe. Tofuati hizi hufuata mpangilio, mwingine zikiruhusu watumizi kupakua vitabu bila malipo, nyingine zina malipo ya muda, il-hali nyingine hulazimu mtu kununua kile kitabu anachokihitaji.
Teknolojia za habari na mawasiliano (ICT) ni seti ya vifaa na rasilimali mbalimbali zinazotumiwa kuwasiliana, kuunda, kueneza na kuongoza habari. Teknolojia hizi ni pamoja na kompyuta, mtandao, teknolojia za kusambaza habari  redio na televisheni, simu kuongea na pia kwa ujumbe wa maandishi yaani (sms). Kuna mvuto unaoongezeka kuhusu namna tarakilishi na mtandao vinavyoweza kuimarisha elimu katika viwango vyote, yaani mseto wa elimu rasmi na ile isiyo rasmi.
Teknolojia za habari na mawasiliano za awali, kama vile redio na televisheni, zimetumiwa kwa zaidi ya miaka 40 kwa elimu wazi na ile ya mbali, hata hivyo kupiga chapa ndiyo njia nafuu zaidi, inapatikana kwa urahisi, na hivyo basi ni mbinu iliyotawala katika nchi zilizoendelea na zile zinazoendelea.
Matumizi ya tarakilishi na mtandao (ikiwa vinatumika) bado ni changa katika nchi zinazoendelea, na hii ni kwa sababu miundo msingi ni michache na ghali. Kwa kawaida teknolojia kadhaa hutumiwa kwa pamoja bali si mbinu pekee ya kupokelewa. Kwa mfano, Kothmel Community Radio Internet hutumia matangazo ya redio na kompyuta pamoja na teknolojia ya mtandao, na hivyo hurahisisha kugawa habari na kutoa nafasi za elimu katika kijiji fulani Sri Lanka.
Chuo Kikuu cha Uingereza (UKOU) kilichoanzishwa mwaka wa 1969 kama taasisi ya elimu ya kwanza ulimwenguni kujitolea kutoa elimu ya wazi na ya mbali, bado hutegemea vifaa vilivyopigwa chapa na kuongezea redio, runinga na kompyuta. Vivyo hivyo, Chuo Kikuu cha Indira Gandhi nchini India huweka pamoja matumizi ya chapa, sauti zilizorekodiwa, video, redio na teknolojia ya vielezo vya kusikiza mkutano.
Dhana ya masomo yanayosaidiwa na kompyuta (CAL) limetumiwa kwa wingi kuelezea teknolojia katika masomo.
Nadharia ya elimu 
Nadharia ya elimu ni nadharia ya azma, matumizi na ufafanuzi wa elimu na kusoma. Historia yake inatokana na wataalamu wa elimu kutoka Ugiriki kuanzia karne ya 18. Katika karne ya 20 mbinu za kusoma zimetumia nadharia katika kufunza, kutathmini na katika sheria za elimu ambazo hupatikana katika vitengo mbalimbali kama ifuatavyo:
Uchumi

Sababu zimetolewa kuwa kiasi cha juu cha elimu ni muhimu kwa nchi ili kuwezesha ukuaji haraka wa uchumi. Uchunguzi unaotegemea nadharia huunga mkono nadharia za kutabiri kuwa nchi maskini zinapaswa kukua haraka kuliko nchi tajiri kwani nchi hizi zinaweza kutumia teknolojia mpya kabisa ambayo imeshajaribiwa na nchi tajiri.
Hata hivyo, kuhamisha teknolojia kunahitaji viongozi wenye maarifa na wahandisi wenye uwezo wa kutumia mashine mpya ama mazoezi ya uzalishaji yaliyokopwa ili kuziba mpaka kwa miigo. Hivyo basi, uwezo wa nchi wa kujifunza kutoka kwa nchi kiongozi ni jukumu la wafanyakazi wa nchi hiyo.
Utafiti wa hivi karibuni wa vitambulishi vya kujumuisha ukuaji wa kiuchumi umesisitiza umuhimu wa vyuo asili vya uchumi na majukumu ya ujuzi tambuzi.
Kazi hii imetia motisha idadi kubwa ya utafiti lakini pia inaelekea kuleta mabishano kwa kiasi fulani. Ubishi mkubwa unahusu jinsi ya kufasiri matokeo ya kusoma.
Saikolojia ya elimu ni uchunguzi wa jinsi watu hujifunza katika mandhari ya elimu, maingiliano ya elimu, saikolojia ya kufunza na saikolojia ya  jamii za shule. Ingawa maneno “saikolojia ya kielimu” na “saikolojia ya shule“ mara nyingi hutumiwa kwa kubadilishana, watafiti na wananadharia wanaweza kutambuliwa kama wanasaikolojia wa elimu, il-hali weledi wanaopatikana shuleni au mandhari yanayoana na shule hujulikana kama wanasaikolojia wa shule. Saikolojia ya elimu inajishughulisha na utaratibu wa kutoa elimu kwa watu na umma kwa jumla na umma mdogo, kama vile watoto wenye vipaji na wale wenye ulemavu.
Saikolojia ya elimu inaweza kueleweka kwa sehemu kupitia masomo mengine. Saikolojia ya elimu vilevile huarifiwa na saikolojia, ikileta uhusiano baina ya utabibu na biolojia. Saikolojia ya elimu pia huarifu masafa mapana ya masomo maalum yakiwemo mpango wa mafunzo. Teknolojia ya elimu, mtaala uliokuzwa, masomo yaliyopangwa, masomo maalumu, sayansi tambuzi na sayansi masomo. Katika vyuo vikuu, idara za elimu ya saikolojia zimehifadhiwa katika vitivo vya elimu. Hii ni kwa sababu ya uwezekano wa ukosefu wa uwakilishaji wa maudhui ya saikolojia ya elimu katika utangulizi wa vitabu vya saikolojia.

Sosholojia ya elimu; ni somo linalohusu jinsi taasisi za kijamii na huathiri michakato na matokeo ya elimu  kinyume chake. Kwa wengi, elimu hueleweka kama mbinu ya kushinda vizuizi, kufanikisha usawa na kupata amani na hadhi kwa wote (Sargent 1994). Wanafunzi wanaweza kutiwa motisha na hamu ya maendeleo na uboreshaji. Elimu hutambuliwa kama mahali ambapo watoto huweza kujikuza kulingana na mahitaji yao ya pekee. Jukumu la elimu linaweza kuwa ni kukuza mtu binafsi hadi kilele. Uelewa wa shabaha na mbinu za michakato ya utangamano wa kielimu hutofautiana kulingana na dhana ya sosholojia iliyotumika.
Katika nchi zinazoendelea idadi na uzito wa shida zilizoko kwa kawaida ni kubwa. Watu wa vijijini wakati mwingine huwa hawana habari kuhusu umuhimu wa elimu. Hata hivyo, nchi nyingine zina wizara ya elimu na katika masomo mengi, kama vile kujifunza lugha za kigeni, kiwango cha elimu kimo juu kuliko katika nchi zilizoendelea. Kwa mfano, katika nchi zinazoendelea ni kawaida kupata wanafunzi wakizungumza lugha nyingi za kigeni kwa usanifu mkubwa, il-hali jambo hili ni nadra katika nchi zilizoendelea ambapo idadi kubwa ya watu huzungumza lugha moja.
Vilevile kuna shinikizo la kiuchumi kutoka kwa wazazi ambao hupendelea watoto wao wapate pesa kwa muda mfupi kuliko faida za elimu ya muda mrefu. Utafiti wa hivi karibuni kuhusu ajira ya watoto na umasikini zimependekeza kuwa familia zilizokumbwa na umasikini zinapofikia kiwango fulani cha kukidhi mahitaji yao ya kimsingi, wazazi huwarejesha watoto wao shuleni. Hii imethibitshwa kuwa kweli mara tu kizingiti kinapovukwa. Hata kama uwezekano wa thamani ya kiuchumi ya ajira ya watoto inaongezeka baada yao kurudishwa shuleni.
Ukosefu wa vyuo vikuu bora na kiwango cha chini cha kukubalika katika vyuo hivi ni dhahiri katika nchi zilizo na idadi kubwa ya watu. Baadhi za nchi zina mitaala mikuu inayoweza kubadilika kwa urahisi, inayofanana na yenye miundo zaidi.
·         Kutokana na utandawazi shinikizo kwa wanafunzi katika shughuli za mtaala zimeongezeka
·         Kuondolewa kwa asili mia fulani ya wanfunzi kwa ajili ya uboreshaji wa masomo; kwa kawaida hufanywa shuleni baada ya daraja la kumi.
India inakuza teknolojia na mtandao. India ilizindua EDUSAT, elimu ya setilaiti ambayo inaweza kuwafikia wengi kwa gharama ya chini. Kuna pia mpango ulioanzishwa na shirika la OLPC, kundi lililotokana na maabara ya MIT lililoungwa mkono na mashirika makuu ili kukuza kompyuta ya kupakata ambayo ingeghalimu $100, ili kuwezesha kuwasilisha elimu ya programu ya kompyuta. Kompyuta hizi zimesambaa kote kufikia mwaka wa 2009. Kompyuta hizi zinauzwa au kutolewa kama msaada. Hii itawezesha nchi zinazoendelea kuwapa watoto wao elimu kwa kutumia mitambo.
Barani Afrika, shirika la NEPAD limezindua programu ya masomo ya mtandao inayotoa vifaa vya kompyuta na masomo ya mtandao kwa shule zote za msingi na upili kwa kipindi cha miaka kumi. Vikundi vya binafsi kama vile Wamormoni, wanajikakamua kuwapa watu fursa ya kupokea elimu katika nchi zinazoendelea kupitia miradi kama vile Perpetual Educational Fund. Mradi wa maendeleo kimataifa inayofahamika kama nabuur.com, com iliyoanza kwa msaada wa rais wa Marekani Bill Clinton, hutumia mtandao kuwezesha ushirikiano wa watu binafsi kuzungumzia maswala ya maendeleo ya jamii.
Elimu inaendelea kuwa jambo la kimataifa. Si vifaa vyake tu vinavyoendelea kuathiriwa na mazingira ya kimataifa yenye ukwasi bali pia mabadiliko ya wanafunzi katika viwango vyote yanayochangia kuendesha jukumu hili muhimu. Kwa mfano kule Uropa, programu ya Socratis Erusmus imechechemua mabadilishano kati ya vyuo vikuu vya Uropa. Vile vile, Shirika la Soros hutoa fursa nyingi kwa wanafunzi kutoka Asia ya kati na Uropa mashariki. Wasomi wengi hudai kwamba ingawa mfumo fulani unaweza kuzingatiwa kuwa bora au mbaya kuliko mwingine, kuzoea aina tofauti ya elimu mara nyingi huonwa kuwa elementi muhimu ya kuzoea masomo ya kimataifa.
Dini na elimu
Elimu katika dini ya Uislamu ni muhimu kwa wake na waume.Kinyume na dhana ya kawaida, kutafuta aina zote za maarifa, yawe ya kitaaluma, ya kidini au ya kidunia yanaruhusiwa kwa watu wa umri wowote. Hata hivyo, masomo ya umri mdogo huonwa kuipa akili fursa ya kumakinika bila kuathiriwa na shida na majukumu ya maisha ya utu uzima.
Moja ya maandiko katika Bibilia yana sema,”Mkamate  elimu usimwache aende zake”. Methali


Kwa maoni, ushauri  na chochote kile ukifikiriacho usisite hapa;;;;;;;;;;
                                           +255767611645
                                           +255715080716
Mwanaharakati1992@gmail.com.

No comments:

Post a Comment

Pages