KAZI ZA MWENYEKITI WA KITONGOJI/MTAA. - waleo blog

Breaking

Wednesday 1 April 2020

KAZI ZA MWENYEKITI WA KITONGOJI/MTAA.


#UTAWALA

Maana ya kitongoji /mtaa.
Kitongoji ni sehemu ya kijiji, mamlaka ya mji mdogo au mamlaka ya mji. Eneo la kijiji linatakiwa kugawanywa katika vitongoji  visivyozidi vitano kulingana na idadi ya kaya na jiografia ya eneo husika.
Mkutano wa wakazi na kitongoji
Mkutano wa wakazi wa kitongoji unahudhuriwa na wakazi wa kitongoji wenye umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea. Mkutano wa kitongoji una mamlaka ya kumchagua na kumwondoa mwenyekiti  wa kitongoji”kisheria”. Mkutano wa  kitongoji hufanyika mara moja kila mwezi ili kujadili  ustawi na maendeleo ya kitongoji. Ila unaweza kuitiswa na mwenyekiti wa kitongoji wakati wowote jinsi atakavyoona inafaa na pindi jambo la dharula lenye manufaa ya kipekee kwa wanakitongoji.
Kazi na majukumu ya mkutano wa wakazi kitongojini.
v  Mbali na mambo mengine, mkutano wa wakazi kitongojini utakuwa na majukumu yafuatayo.
·         Kupokea na kujadili taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo ya kitongoji kama zitakavyowasiliswa na mwenyekiti wa kitongoji.
·         Kujadili taarifa za utekelezaji wa mikakati ya kupambana na umasikini.
·         Kujadili hali ya ulinzi na usalama na maendeleo katika kitongoji.
·         Kuweka mikakati kupambana na ugonjwa wa UKIMWI.
·         Kupokea maelekezo kutoka Halmashauri ya kijiji na kuweka mikakati ya utekelezaji wake katika kitongoji.
Kazi za mwenyekiti wa kitongoji
Mwenyekiti wa kitongoji  atakuwa na kazi zifuatazo;
·       Kuitunza rejesta/takwimu/idadi ya wakazi wa kitongoji  na habari nyingine muhimu zinazohusu maendeleo  ya kitongoji  kwa jumla, ikiwa ni pamoja na kumbukumbu za vizazi na vifo.
·        Kusimamia shughuli za ulinzi na usalama wa watu na mali zao waishio katika eneo lote la kitongoji.
·        Kuhamasisha ulipaji wa kodi na ushuru mbalimbali, kama utakavyoamuliwa na kuwekwa mara kwa mara na halmashauri ya wilaya, mji, manispaa au jiji.
·        Kusimamia katika eneo lake suala zima la hifadhi ya mazingira hususani vyanzo vya maji, misitu nk.

·       Kusimamia suala la afya katika eneo lake ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa kampeni za afya za kitaifa, kimkoa au kiwilaya dhidi ya magonjwa  ya kuambukiza, na hasa vita dhidi ya UKIMWI na ya mlipuko.
·        Kusimamia utekelezaji wa kanuni za kilimo na ufugaji bora ili kuinua hali ya lishe na uchumi wa wakazi wa kitongoji.
·        Kufuatilia na kuhakikisha kuwa kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule anapatiwa nafasi na kushirikiana na viongozi wa shule katika kudhibiti utoro shuleni.
·        Kuhamasisha elimu ya watu wazima(ngumbaru).
·        Kusimamia na kuwahamasisha wakazi wa kitongoji katika kutekeleza  shughuli za kujitegemea .
·        Kusuluhisha migogoro midogo midogo isiyostahili kushughulikiwa na baraza la kata na mahakamani.
·        Kuwakilisha kitongoji katika serikali ya kijiji.
·        Kuwaongoza na kuwahamasisha wakazi wa kitongoji washiriki katika sherehe za taifa na mikutano ya hadhara itakayoandaliwa na kuitishw serikalini au halmashauli.
·        Kutekeleze kazi nyingine atakazopangiwa na halmashauli ya kijiji, wilaya, mji, manispaa au jiji.
·        Mwenyekiti anaweza kuteua kamati ya ushauri yenye wajumbe wasiozidi watatu ambao ni wakazi wa kitongoji hicho kwa ajili ya kushauri juu ya mambo mbalimbali yenye maslahi kwa kitongoji kinachohusika.

Hizo ni kazi kuu za mwenyekiti wa kitongoji/mtaa.
Baki nasi kwa vizuri vijavyo.

Kwa ushauri na chochote kile kilichokukwaza na kukufurahisha nk, usisite kutucheki hapa:                  
                   +255767611645
                   adamgome96@gmail.com
                   +255715080716
                   Mwanaharakati1992@gmail.com

No comments:

Post a Comment

Pages