SUMU YA NGE NI DILI. - waleo blog

Breaking

Wednesday 25 March 2020

SUMU YA NGE NI DILI.


#UTALII

Nge;asili ya neno hili ni kwa kutoka katika lugha ya kiarabu,’AQRABU” Spishi hizi ndogo huitwa visusuli. Ana miguu minane. Mkia wake ni mrefu na una msumari mkubwa mwishoni mwake. Kama kawaida kiwiliwili chake kina sehemu mbili: kefalotoraksi ( cephalothoraxkichwa na kidari) na fumbatio lakini zimeungwa kwa upana, siyo kwa pediseli (nyembamba lenye umbo la mrija kama kwa buibui. Mgongo wa kefalotoraksi ni mgumu na kwa hivyo, huitwa gamba. Nge wana macho 6-12, mawili juu ya gamba la kefalotoraksi na 2-5 kwa kila upande wa kichwa. Msumari wa nge hutumika kwa kudunga windo na kuingiza sumu ndani yake. Windo akiwa amekufa, kelisera za nge zinakata vipande vidogo vinavyowekwa katika kishimo mbele ya mdomo. Maji ya umeng'enyaji yakamuliwa katika kishimo hiki na baada ya kumeng'enya chakula; myeyuko ufyondwa. Nge hula arithropodi wengine na wale wakubwa hula mijusi na vipanya wadogo pia.

Faida ya sumu ya nge


Kabila moja nchini Afrika ya kusini  ambalo huishi porini, huchanganya sumu hiyo ya nge na pombe ya asili kwa lengo kutibu mgonjwa yaliyopo mwilini.
Leo tuishie hapa.Itaendelea_,_,_,_,….


Ushauri ni hapo.
                                                +255767611645
                                                +255715080716

No comments:

Post a Comment

Pages