MISINGI BORA YA KIJANA. - waleo blog

Breaking

Wednesday 1 April 2020

MISINGI BORA YA KIJANA.


#MALEZI


KIJANA NI NANI?      
Kijana ni rika kuanzia  miaka kumi na tano {15} hadi arobaini {40}.Baadhi ya wataalamu wa elimu ya upevukaji huamini ya kuwa, ujana ni pale tu mtu atakapoanza kuonesha dalili za ukuaji yaani kubalehe hadi miaka arobaini na tano . wataalamu hawa huamini ya kuwa miaka hii ya 45,mtu huanza kupunguza uwezo wa kufanya kazi zote zilizokuwa zikifanywa alipokuwa kijana mfano,uwezo wa kufikiri na kutunza kumbukumbu. Leo katika makala hii nimeona nikuletee machache yahusuyo misingi bora ya kijana kama ifuatavyo.

Mchapakazi; kijana yeyote yule anaejielewa juu ya safari yake ya maisha yaani, anakotoka na anakoenda  basi nilazima ahakikishe anafanya kazi  kwa bidii ili kuhakikisha anafika malengo yake. Wapo baadhi ya vijana hujihakikishia maisha bora na il-hali hana shughuli yeyote ya kiuchumi anayoifanya, “Hili nalo ni tatizo la kiakili, wasaidiwe hawa “.

Utu; vijana wengi hudhani ya kwamba rika  alilo nalo ni lakufanya fujo zote katika dunia ,!!. Hapana huu si msingi wa kijana mwema ambaye anatarajiwa na wengi kwa matumaini mbalimbali. Utu  ndio heshima na adabu ambamo ndani yake kunapatikana vitu kama kujitolea na kujitoa mfano,kusaidia wadogo kwa wakubwa awesavyo na kujitoa katika mambo ya kijamii. Kijana bora lazima awe na……

Utii; Utiifu kwa wazazi wako, utiifu wa sheria mbalimbali kama vile sheria za nchi , nyumbani, kazini  na hata sheria zako binafsi ni lazima uzitii na kuziheshimu ili kufanikisha mambo mbali mbali. Baadhi ya vijana hushindwa kuwaheshimu na kuwatii wakubwa kwa wadogo, huo si msingi  wa kijana bora. Haipendezi kwa kijana kuwafokea na kuwatukana wakubwa wala wadogo, isipokuwa misingi ya kijana bora huonesha njia bora ya kuwaelekeza wote waliomkosea na kuwakosea kasha kuwaomba/kuomba msamaha.Wapo baadhi ya vijana huondosha utii kwa wazazi wao, kwa sababu mzazi /wazazi wake kushindwa kumtimizia mahitaji yake muhimu kama kumsomesha na kijana huyo huona ugumu wa maisha aliokuwa nao ni kwa sababu ya kukosa elimu huku watu  aliosoma nao wakiwa kama kielelezo cha maisha bora walionayo. “Usilitazame kwa ubaya na kulifyonya/kufonya jiwe ulilo likwaa kisha likakuangusha,bali yatazame kwa umakinifu yale ya mbele yakumezeayo mate”.  Saad S.Dunga    mwandishi.

Tamaa; misingi ya kijana bora ni lazima kuwa na tamaa chanya ya kupambana kwa njia za  halali na salama kumzidi yule ambaye amemtamani na alivyovitamani. Msingi huo utamfanya kuwa na mafanikio mazuri katika jamii yake na kumuepushia lawama baada ya kupitwa na muda.

Mila; kijana bora ni lazima awe mrithi wa mila mbali mbali kutoka kwako na hata sehemu zingine duniani. Kinachotushinda vijana ni kupupia mila na desturi ambazo maadili yake katika jamii  zetu zina muonekano mbaya mfano, mila za wageni  wengi wa mataifa ya Ulaya kuvaa heleni kwa wanaume. Huu si muonekano wa kijana bora. ‘’Tubadilike’’heleni ni moja ya pambo kwa wanawake. Kijana bora ni lazima aepukane na mila na desturi za ulevi,kwa sababu ulevi  hupunguza heshima na si katika misingi ya kijana bora.’’Unalo hilo!!!?, badilika’’. Ili misingi bora yote hiyo iweze kusimama katika ubora wake yampasa kijana awe-


Mcha mungu; ucha mungu ni hali ya kuwa mnyenyekevu na utiifu kwa amri na makatazo yote  aliyoyakataza MWENYEZI MUNGU. Kimsingi huu ndio msingi mama wa misingi ya kijana bora.Ucha mungu huu ni kwa wale waaminio  visivyoonekana kwa macho.’’Fikiria uwezavyo’’.


Ili kijana awe na misingi bora na sio bora misingi , basi hutatikana /anapaswa kuchagua sehemu pa kuishi palipo sahihi na anachokihitaji katika misingi yake mema. lakini pia makundi sahihi ya kushirikiana nayo  katika shughuli zake. Tuwaandae vijana wetu kaika malezi ya kiMungu.
Tunaipongeza serikali yetu ya Tanzania kwa kuzuia baadhi ya vilevi, lakini pia ingefanikisha/kuamua kupiga marufuku kwa vilevi vyote viaribivyo akili, huenda tungefanikisha kuwapata vijana waliokuwa madhubuti wa kuijenga inchi yao kikamilifu zaidi. Mungu ibariki dunia, Mungu ibariki Tanzania na viongozi wake wooote.Lakini pia tunakuomba Mungu wa haki utuepushie majanga makubwa kama ya Maradhi yatishayo na majanga makubwa ya kiasili.Amina


Tafadhali ishee na wengine wapate faida nao.
Maoni na ushauri hapa,  
                                          0767611645
                                          0715080716
                                          mwanaharakati1992@gmail.com
                                     adamgome96@gmail.com


1 comment:

Pages