ZIJUE ATHARI ZA NYAMA NYEKUNDU - waleo blog

Breaking

Sunday 2 February 2020

ZIJUE ATHARI ZA NYAMA NYEKUNDU



#AFYA

Miili yetu inahitaji protini ili kujijenga pamoja na kujenga kinga ya mwili. Vyakula vya protini vinatia ndani nyama, samaki, kuku, kunde, maziwa n.k Watu wengi huamini nyama na maziwa kama vyakula vyenye protini na virutubisho. Na wengi hudhani kula vyakula hivi huonesha hali nzuri ya kiuchumi.
Nyama nyekundu ni pamoja na ng’ombe, mbuzi, kondoo na sungura. Utafiti wa hivi karibuni kuhusu protini unathibitisha kwamba kula nyama nyekundu kunaweza kuhusishwa na hatari kubwa ya kifo.
Tafiti zinaonesha kuwa nyama nyekundu ikitumika kwa wingi ni kati ya vyakula vinavyosababisha aina mbalimbali za saratani kama ile ya kinywa, koo, utumbo mpana, mapafu na kongosho. Pia ina lehemu kwa wingi ambayo huweza kuongeza hatari ya kupata magonjwa ya moyo, shinikizo kubwa la damu, saratani, kisukari na kiharusi.
Kama unatumia nyama nyekundu inashauriwa isizidi nusu kilo kwa wiki. Inashauriwa kutumia zaidi nyama nyeupe, ambayo ni  kuku, bata mzinga na samaki nk. Hata hivyo, kutumia protini inayotokana na mimea badala ya protini inayotokana na wanyama katika mlo wako huhusishwa na upungufu wa hatari ya kifo.

Wanasayansi kwa muda mrefu wamehusisha nyama nyekundu ya kusindika na wigo mpana wa magonjwa sugu, kama vile saratani, kisukari na ugonjwa wa moyo.
Utafiti mpya unaonyesha kwamba bado uhusiano huo upo wakati ukichunguza ulaji wa protini kwa ujumla.
“Ingawa ni muhimu kujua ni kiasi gani cha protini watu wanapaswa hutumia ili kufaidika kiafya, kuhusu suala la lishe, watu kutambua ni aina gani ya vyakula wachague ili kupata protini ni suala la muhimu pia”.
Watafiti waligundua kuwa uhusiano kati ya ulaji protini na hatari ya kifo uliambatana na maradhi au kuishi angalau moja ya maisha yasiyokuwa ya kiafya kama vile kuvuta sigara, kunywa pombe kupita kiasi, kiribatumbo au kutofanya mazoezi.
Ongezeko la asilimia 10 katika ulaji protini za wanyama umehusishwa na ongezeko la asilimia 2 la vifo kiujumla na ongezeko la asilimia 8 la hatari ya kifo kutokana na maradhi ya moyo na mishipa.
Hata hivyo, kuongezeka kwa asilimia 3 katika ulaji protini ya mimea kumehusishwa na asilimia 10 ya kupungua kwa vifo kwa ujumla na asilimia 12 ya kupungua kwa vifo vitokanavyo na maradhi ya moyo na mishipa.
Mtafiti mmoja wa tiba lishe anasema, ulaji protini za wanyama umekuwa ukihusishwa na kiwango cha juu cha insulini ya ukuaji kipengele cha kwanza, protini ambayo imekuwa inahusishwa na matokeo mabaya ya afya, ambapo ulaji mwingi wa protini ya mimea umekuwa ukihusishwa na kushusha shinikizo la damu na kuboreka usikivu wa insulini.
Anasema inawezekana kwamba virutubisho vingine katika vyakula zaidi ya protini vinaweza kusababisha madhara, mfano nyama nyekundu zilizosindikwa huwa na sodiamu nyingi, nitriti na nitrati, ambazo zote zimekuwa zikihusishwa na matokeo mabaya ya afya.
Mfano wa nyama hizo ni soseji, nyama za kopo, hotdog, salami na bacon.
Inashauriwa kuepuka kutumia nyama zilizosindikwa au kuhifadhiwa kwa chumvi, mafuta, kemikali au kukaushwa kwa moshi. Nyama zilizosindikwa zimethibitishwa kuongeza hatari ya kupata saratani hata zikitumiwa kwa kiasi kidogo tu.
 Vyakula vyenye protini ya mimea kwa wingi
Wanasayansi bado hawajapata kipimo,yaani hawana uwezo kwa sasa wa kugundua kama mtu anatumia aina gani ya protini kati ya protini ya wanyama na protini ya mimea, wangeweza kufanya hivyo wangesaidia kutoa uelewa mzuri kwa jamii juu ya jinsi gani vyakula hivyo husababisha vifo vya watu.
Vyanzo vizuri vya vyakula vyenye protini ya mimea ni pamoja na mikate ya ngano isiyokobolewa, nafaka zisizokobolewa, karanga, maharagwe ya soya na kunde.
TANBIHI: kwa sasa watu wengi husumbuliwa na ugonjwa wa magoti au sehemu za viungio vya mwili yaani dalili za malaria,uti ama typthod na kuchukua hatua za kutibu na,baada ya siku maumivu yako pale pale. Hizo ni dalili za ugonjwa wa Bruccelosis unaosababishwa na ulaji wa nyama nyekundu kupitiliza.Epuka na chukua hatua kasha jitibie.Wataalamu wanasema ya kwamba ugonjwa huu wa gaut ukipuziwa, basi humpelekea mtu kuwa chizi.Hivyo basi uonapo dalili hizo chukua tahadhari na uanze tiba.





No comments:

Post a Comment

Pages