JE! UNA WAZAZI/MZAZI? WAFANYIE HIVI. - waleo blog

Breaking

Sunday 2 February 2020

JE! UNA WAZAZI/MZAZI? WAFANYIE HIVI.


#WOSIA

Tafadhali, huenda baadhi ya maneno yasikupendeze utusamehe, lengo ni kukumbushana ili jamii ibadilike.
HADITHI ZA KWELI.
Amesimulia mtoto wa omari ya kuwa, mtu mmoja alikuja kwa kipenzi cha mungu wa zama zilizopita, (rehema za Mungu na amani zimshuke) akasema: “Nimekuja kukupa ahadi ya utii juu ya  kuhama pamoja nawe kwenda kupigana vita juu ya maisha yetu ya baadae”Kipenzi cha mungu yule  akamuuliza yule kijana: “Je, kati ya wazazi wako wawili yupo aliye hai?” Akasema kijana: “Ndio, wote wapo hai.” Kipenzi akamuuliza: “Je, unatafuta ujira mkubwa kutoka kwa Mungu wako?” Akajibu kijana yule: “Ndio.” Kipenzi wa mungu akasema: “Rudi nenda ukawafanyie wema wazazi wako.”watu wawili walishuhudia tukio hili la kweli..
Katika dini Fulani nimewahi kusikia wakisema; wazazi wamepewa nafasi, uzito na heshima ya kipekee. Mwenyezi Aliyetukuka anasema: “Na Mola wako mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata ‘Ah!’. Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa heshima. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme, ‘Mola wangu mlezi! Wahurumie wazazi wangu kama  walivyonilea utotoni.” (Injili, Zaburi na Furukan, 17:23-24).
Hapa Mungu aliyetukuka anawakumbusha watoto kuwafanyia wema na ihsani wazazi wao, kwa kuwa hiyo ni ibada inayopendwa na kuridhiwa na yeye. Mwenyezi Mungu aliyetukuka nautukufu wake ameahidi malipo makubwa duniani na mbinguni kwa yeyote atakayechunga haki za wazazi wake wawili na kuwaheshimu. Ni ubaya ulioje kwa mtu anayepuuza jukumu hili.     ’’Na aamini mwenye kuamini’’ methali za sulemani.
Namna ya kuwafanyia wema wazazi
Kuna namna nyingi za kuwafanyia wema wazazi. Miongoni mwa hizo ni kuitika wito wao na kutekeleza mahitaji yao kadiri inavyowezekana  pia  kuwapa heshima na hadhi ya juu. Usiwe mwenye kuwatembelea wazazi wakati wa  matukio maalumu,kama vile siku za sikukuu, bali watembelee mara kwa mara na ujipendekeze kwao.

Namna nyingine za kuwafanyia wema wazazi wawili ni  kuwashauri katika mambo mbalimbali na kuthamini ushauri wao, kuwaombea mema kila wakati, kuwahimiza kudumisha mambo mbalimbali ya kheri kadiri watakavyoweza, kuwaheshimu wakati wote na katika mazingira yote, mbele za watu, hata mkiwa peke yenu.
Watunze wazazi wako kadiri inavyowezekana na kamwe usiwatelekeza au kuwaacha wafanyakazi wawahudumie pasi na juhudi zako kuonekana. Vilevile, waheshimu wazazi wako na uwaoneshe watu kuwa hiyo ni tabia yako na si maigizo.
Mambo yasiyofaa kufanyiwa wazazi
Haifai kuwaliza au kuwahuzunisha wazazi, iwe kwa kauli au vitendo. Hilo ni jambo baya mno mbele ya mwenyezi Mungu. Haitakiwi mtoto awe  ndio chanzo cha wazazi wake kutokwa na machozi. Pia, ni dhambi kuwakemea, kuguna, kukiuka amri yao halali kwa Mungu na maelekezo yao,  kuwakunjia uso au kunyanyua sauti juu yao.
Ni ukweli kuwa; wapo baadhi ya watu wanaoonesha nyuso za bashasha kwa watu wengine lakini wanawakunjia uso na kuwakasirikia wazazi wao na kuwatazama kwa dharau hususani pale wanapowataka wawasaidie kazi au majambo mbalimbali.
Haifai, na pia ni haramu kubishana na wazazi, kuwatukana, kutowashauri katika mambo mbalimbali, kutothamini  mawazo yao, kuingia chumba au nyumbani mwao bila hodi, kuwavunjia  heshima kwa kufanya vitendo viovu kama wizi, kutukana au kuanzisha ugomvi na ndugu na jamaa zao. Kufanya hayo kunaweza kuwaingiza wazazi wako katika tuhuma mbalimbali na hivyo kuishi na majonzi na huzuni. ‘’Jiepushe’’
Pia, haifai kuwalipisha wazazi madeni yasiyowahusu au kufanya kosa litakalopelekea aitwe shule, chuo ama sehemu yoyote ile ambayo itakua na usumbufu kwao kwa sababu yako tena kwa makusudi.Hafai kutaja aibu zao mbele ya watu wengine, kuwalazimisha wakununulie vitu wasivyo na uwezo navyo, kumfadhilisha mke juu yao, kuwapeleka kwenye nyumba za kulelewa wazee wakati una uwezo wa kuwahudumia, kuwafanyia ubakhili na kufanya masimbulizi, yaani  kuhesabu mema uliyowafanyia.
Ukaishi hivi na wazazi wako, basi kwa hadithi ileee niliowahi kuisikia nikipita sehemu Fulani,wewe ni wa peponi kwa wale waaminio kwayo, na kitakacho kuchelewesha kwenda huko Paradaise yaani peponi ni kifo tu.Tujitahiidi ndugu zangu.
Share kwa wingi ili watu wakumbuke,waelewe ili wazazi nao wale Bata(vitu vizuri ) za watoto wao.

No comments:

Post a Comment

Pages