WAJUE NGURUE MWITU NA KAYA - waleo blog

Breaking

Wednesday 19 February 2020

WAJUE NGURUE MWITU NA KAYA


#Utalii

Ngirigwasi au mbango  ni wanyama wa jenasi  katika familia Suidae. Hizi ni aina za nguruwe-mwitu wenye sugu kubwa kichwani, madume hasa (sababu ya jina kwa Kiingereza: warthog). Wana pamba ndefu, zile za dume ndefu kuliko zile za jike. Hula manyasimiziziberi na matunda mengine, gamba la miti, nyoga na hata mayaimizoga na pengine wadudu na wanyama wadogo. Wakila hupiga magoti ya mbele na wakitoroka kitisho huweka mkia juu wima.

Nguruwe ni wanyama wa familia SuidaeNguruwe-kaya hufugwa kote duniani. Spishi mbili zinaitwa ngiri.


Tabia na maelezo
Nguruwe ana pua kubwa, macho madogo na mkia mdogo unaokuwa umejikunja na mfupi, uliopinda au ulionyooka. Huwa ana mwili mkubwa, miguu mifupi na nywele zilizojiviringisha. Ana kwato nne kwa kila mguu, huku mbili kubwa za mbele zikitumika kutembelea.
Kuzaa huwezekana msimu wote wa mwaka katika ukanda wa tropiki, lakini hasa misimu ya mvua. Nguruwe jike huweza kubeba mimba akiwa na miezi 8 mpaka 18. Kisha ataanza kupata hedhi kwa muda wa siku 21 kama hajashika mimba. Nguruwe dume huweza kushiriki masuala ya uzazi katika umri wa miezi 8 mpaka 10. Kwa uzao mmoja, wanaweza kupatikana watoto 6 mpaka 12, waitwao vibwagala. Kisha kuachishwa kunyonya, familia mbili au tatu zinaweza kuishi pamoja mpaka msimu mwingine wa kujamiiana.
Nguruwe hawana tezi za jasho, hivyo nguruwe hujipoza kwa kutumia maji au matope wakati wa joto kali. Pia hutumia matope kama njia ya kujikinga na kuunguzwa na jua. Zaidi, matope huzuia wasiathiriwe na inzi na vijidudu.
Nguruwe wanaofugwa nyumbani hukuzwa na wakulima kwa ajili ya nyama na ngozi. Nywele zao ngumu hutumika pia kwa kutengeneza brashi. Baadhi ya spishi za nguruwe, kama vile wale wa Asia,  huwekwa kama wanyama wa ndani wapenzi.

Chakula
Nguruwe ni omnivora, yaani wanakula nyama na majani. Nguruwe hula mabaki na hujulikana kwa kula chakula chochote, kujumuisha wadudu, minyoo, magamba ya miti, takataka na hata nguruwe wengine. Wakiwa mwituni hula majani, nyasi, mizizi, matunda na maua. Kwa nadra, nguruwe wakiwa wanafugwa, huweza kula watoto wao kama wakichukizwa sana.
Nguruwe wa kawaida wana kichwa kikubwa chenye pua ndefu iliyoimarishwa kwa mfupa mgumu na mduara wa tishu ngumu mbele. Pua hiyo hutumika kuchimba udongo ili kutafuta chakula na ni ogani yenye uwezo mkubwa wa kuhisi.
Nguruwe huwa na seti kubwa ya meno 44. Meno ya nyuma yametoholewa kusaga, na huendelea kukua na huchongwa na misuguano ya meno yenyewe.
Nguruwe wanaochungwa mwituni kwa msaada wa wachungaji, wana uwezo mkubwa wa kunusa, na hutumika kutafuta uyoga katika nchi nyingi za Ulaya.
Nguruwe wa nyumbani hutambulika kwa jina la kisayansi Sus scrofa. Walianza kufugwa karibu miaka 5,000 mpaka 7,000 iliyopita. Walizaliwa na rangi ya kahawia na kuendelea kuwa wa kijivu. Meno chonge ya juu huwa kama ndovu za kipekee zilizopinda nje na kuelekea juu. Urefu wa nguruwe huweza kufikia milimita 900 – 1800 na uzito wa kg 50 – 350.
Nguruwe wana akili na huweza kufundishwa kazi na mbinu ndogondogo. Hivi karibuni, wamefurahia kupewa nafasi kama wanyama kipenzi wa ndani na, hasa wale nguruwe wadogo.

Huyo ni Ngurue/kiti moto kwa lugha zetu za mtaani .kwa uchache tufuatilie ufaidike zaidi

No comments:

Post a Comment

Pages