KWA NINI WAGANGA HAWATAKI SAMAKI? - waleo blog

Breaking

Wednesday 19 February 2020

KWA NINI WAGANGA HAWATAKI SAMAKI?




1:Asubuhi  kumekucha,  mwili  wangu  patashika,

Swali   hulala na kucha,  kipi  mwili  wangu  fika,

Punde  kutakapo  kucha,  kwa  mganga nitafika,

Waganga wetu  wa  visa samaki  kutowataka.



2 : Habari  nilipopata,  mapema nikajongea,

Hodi hodi nikapita, kwa nanga  nikasogea,

Matatizo nikaleta,yaliyokuwa sumbua,

Waganga wetu wa visa,  samaki  kuto wataka.



3: Tatizo  langu  kupona, mbuzi  nanga  kumtaka,

Wezo wangu  patikana,  samaki  wa maji  taka,

Nanga  nae  nitukana,  samaki  nikipeleka,

Waganga  wetu  wa visa,  samaki kutowataka.



4:  Mizimu  hi  haitaki,  shombo  shombo  huwakera,

Tiba yako  si  samaki,  kubwa   buzi  karakara,

Kama  tiba huitaki,  barabara  hiyo  ng’ara,

Waganga   wetu  wa  visa,  samaki  kutowataka.

No comments:

Post a Comment

Pages