JIJUE/MTAMBUE MWANAO, KUWA MJAMZITO - waleo blog

Breaking

Sunday 2 February 2020

JIJUE/MTAMBUE MWANAO, KUWA MJAMZITO



#AFYA

Kuna baadhi ya wanawake wenye kuonesha dalili za mimba punde tu katika wiki kadhaa baada ya kushika mimba. Kuna maswala mengi kuhusu upataji mimba na ni siku gani mwanamke anaweza kupata mimba. Hebu tujadiliane kwa ufupi. Hedhi yaani mensturation period, ni wakati mwanamke anaweza kujua ya kuwa hana mimba.

Damu inayotoka wakati huu huwa nyekundu. Damu hii hutoka kila mwezi kwa wanawake walio na  mzunguko wa kawaida. Pia damu hii huchukua siku tatu hadi tano kwa wale wenye mzunguko wa kawaida. Unapokosa hedhi, baada ya siku kadhaa kupita uliposhiriki tendo la ndoa kwa wana ndoa na ngono kwa wazinifu, kuna dalili kubwa ya kuwa umeshika mimba.

Ni vyema kujua jinsi ya kujichunga ili wewe na mwanawe muwe salama. Hata kabla ya kukosa hedhi (mensturation/period). Unaweza kudhani au kutumai una mimba. Tumaini ni kwa wale wanaopenda kupata watoto. Wakati mwingine, mimba huja na hofu, haswaa ukiwa umefanya mapenzi kando ya ndoa. Lakini usitie shaka, mtoto ni baraka na ni lazima na wajibu wa kila mzazi kujua wanapotarajia mwana.

Dalili za mimba kwa wanawake wengi huonyesha katika wiki za kwanza wanapopata mimba. Hizi dalili ni tofauti kwa kila mwanamke. Kuna wale ambao huwa na machungu na magonjwa zaidi ya wengine na kuna wale wanaopitia hali hii kwa njia rahisi mno.

Swali ambalo kila mwanamke anaweza kuwa nalo ni, Je ninaweza kushika mimba wakati nina hedhi?
Jibu la hakika ni ndiyo! Ingawaje wanawake wengi hawawezi kushika mimba wakati wana hedhi. Kuna baadhi ya wengine wanaoweza kushika mimba wakati wanashiriki mapenzi  hedhini. Hii si kawaida kwa wengi lakini kulingana na dakitari Jeannnette Lager, M.D, MPH aliyesomea maumbile ya wanawake, anatueleza jinsi mwanamke anaweza kushika mimba wakati ana hedhi, sana sana kwa wale walio na mzunguko mfupi zaidi yaishirini na nane.
Haya basi hebu tufafanue zaidi juu ya ugunduzi ya kuwa umeshika mimba.

Dalili zifuatazo za mimba ni maagizo tu ya kuelewa jinsi unavyoweza kukumbatia hali yako ukiwa na mimba.

  • Kukosa Hedhi (Missed Period)
  • Utoaji damu mwepesi (light spotting/implantation bleeding)
  • Kufura kwa Matiti (swollen Breasts)
  • Mhemko wa hisia (Mood swings)
  • Kutoa hewa ( lots of gas)
  • Kutapika au kuhisi kutapika (Nausea and vomiting)
  • Kufura tumbo (bloating)
  • Kukojoa kila wakati (frequent urination)
  • Constipation (Kuvimbika)
  • Mgongo kuuma upande wa chini (lower back pain)
  • Kuumwa kwa kichwa (headache)
  • Kuzidi joto (increase of basal temperature)
  • Uchovu (fatigue)
  • Kutamani aina ya vyakula (food cravings)
  • Kulia (crying)
  • Kulala mara kwa mara (sleepiness)
Urahisi na kufura Matiti
Matiti yako yanaweza kuonesha dalili za kwanza ya mimba. Wiki mbili baada ya kupata mimba, mabadiliko ya homoni yanaweza kufanya matiti yako kuwa makubwa kuliko kawaida, unaweza kuhisi kujikunakuna na uchungu kiasi, pia unaweza kuhisi kama matiti yako yamejaa au mazito.

Uchovu
Uchovu umekuwa hali na dalili ya kwanza mno kwa wanawake wajawazito. Homoni inayoitwa Progesterone huongezeka kwa wingi na inaweza kukufanya kuhisi usingizi kila wakati. Pia upunguzaji wa sukari katika damu, upunguzaji wa shinikizo la damu (blood pressure) na uzidishaji wa damu unaweza kukufanya uwe mchovu wakati wa mimba.


Utoaji damu nyepesi na uchungu kwa tumbo la uzazi
Kuna wakati, damu mwepesi (spotting) huwa dalili ya mimba mapema. Damu hii huwa nyepesi mno na haiwezi kulinganishwa na ile ya hedhi. Rangi ya damu hii ni waridi au kahawia kulingana na hali ya mwanamke. Wakati mbegu ya mwanaume na zile za mwanamke zinapokutana kumtengeneza mtoto, mwanamke anaweza kutoa damu nyepesi kuonesha ya kwamba mwana amelazwa vyema katika tumbo la uzazi wa mwanamke.
Damu hii huchukua siku chache sana kutoka kulinganishwa na ile wa hedhi. Kuna wanawake wengine wenye hukosa kuonesha damu hii nyepesi wanapopata mimba. Sio lazima wanawake kutokwa damu wanaposhika mimba.  ni muhimu kuelewa ya kuwa mwili wa kila mwanamke ni tofauti. Pia, uchungu katika tumbo la uzazi wakati mimba hutengenezeka, unaweza kufanana na ule wa hedhi.

Kuhisi kutapika
Ugonjwa wa asubuhi (morning sickness) unaweza kufanyika wakati wowote wa siku. Kuna wanawake waliosemekana kubeba mimba ambao huwa na ugonjwa huu hivi punde wanapoamka. Kuna wengine wanaopata ugonjwa huu wakati wa mchana na wengine wakati wa usiku. Kila mwanamke ana utofauti kulingana na maumbile ya mwili wake.
Wanawake wengi kwa jumla hupata (morning sickness) wiki mbili wanaposhika mimba. Kutapika huwa matokeo ya homoni inayoitwa estrogen inapoongezeka mwilini. Kuna wanawake wengi ambao hunusa harufu za aina mbali mbali, kama vile marashi, vyakula mbali mbali kama mayai, kwa haraka na pia harufu zingine huwafanya kuhisi kutapika.
Ukiwa unahisi kutapika, unaweza kula au kunusa ndimu au kula matunda kama ndimu, mizizi kama tangawizi na pia kuhakikisha una kunywa maji mengi kwa wakati huo.
Kuna wanawake wengine husema wanaweza kuhisi ladha ya chuma ulimini mwao. Haya yote ni kwa sababu homoni estrogen imeongezeka mwilini baada ya  mimba.
Kutamani vyakula vya aina  au Kukataa
Ukiwa umeshika mimba, unaweza kutamani vyakula fulani, ilhali kuna vyakula mbali mbali ussivyovipenda.
Kuna wanawake wengi waliopenda mayai na sasa hata harufu ya mayai huwafanya kutapika. Na kuna wale wanaoanza kupenda matunda au vyakula  vya aina mbali mbali wanapokuwa wajawazito.
Haya yote ni kwa sababu ya mabadiliko ya homoni mwilini, haswa kwa muhula wa kwanza mwezi mmoja hadi mitatu ya mimba. Pia unaweza kuhisi njaa wakati wowote wa siku. wanawake wengi ulimwenguni huanza kula zaidi ya kawaida na hii ni ishara kubwa ya kwamba mwanamke amepata ujauzito.

Kuvimbiwa (constipation)
Hali ya kutoenda haja kubwa ni kawaida kwa mwanamke yeyote aliye na mimba. Dalili hii ni ile kati ya kwanza wakati mwanamke amepata ujauzito. Homoni Progesterone hufanya chakula kuenea polepole kwenye matumbo na hii husababisha ugumu wa kuenda haja kubwa.

Mhemko wa hisia
Katika muhula wa kwanza wa mimba, utaweza kupata mhemko wa hisia. Unaweza kuhisi furaha halafu baada ya muda mchache wahisi huzuni. Kuna wakati mwingine unaweza kujikuta unalia kwa mambo madogo sana. Haya yote ni kwa sababu mwili wako unapitia mabadiliko kuweza kumtengeneza mtoto.

Kuhisi Kizunguzungu
Wakati damu linaongezeka na shinikizo la damu kupunguza, unaweza kusikia kichwa chepesi au kizunguzungu wakati wa kwanza kama dalili ya mimba. Wakati mwingine, ukosefu wa sukari kwa damu unaweza kufanya mwanamke mja mzito kuzirai.
Ni muhimu wakati unaposikia uwepesi wa mwili, kuketi chini au kujilaza na kuweka miguu juu ya mto ili damu iteremke kichwani. Pia kuhakikisha unakula kila wakati uhisipo njaa; hii husaidia kupunguza hali hiyo.

 Kuhisi Joto  kali
Unapoamka, joto la mwili wako huwa la kawaida kila siku. Unapopata mimba joto hili hugeuka na kuwa jingi kuliko kawaida. Baada ya kuwa na hedhi, kuna wakati mwanamke huwa tayari kupata mimba wakati huu, joto la mwili huongezeka halafu hurudi  kuwa la kawaida baada ya wiki mbili.
Ukigundua kuwa joto hili halijapungua baada ya wiki mbili, basi una dalili kubwa  kuwa na mimba  kama umeshiriki ngono bila kinga.

Kukosa hedhi
Baadhi ya dalili nyingi mwilini mwa mwanamke aliye na mimba, kukosa hedhi ni ile wa kwanza mno haswaa kama (Period) yako ni ya kila mwezi. Utaweza kugundua umekosa mwezi wakati unapojua vyema umefanya ngono bila kujikinga.

Kujawa na hewa
Ni kawaida kwa mwanamke aliye na mimba kuhisi kana kwamba amejaa hewa tumboni na pia kutoa hewa hapa na pale (kujamba). Hii ni kwa sababu tumbo la uzazi linapanuka kuhakikisha mtoto yuko na mahali pa kukua na kuzunguka.
Kuongezeka kwa hamu ya kula
Wanawake wengi wanapopata mimba, ingawaje wengi wao huwa wagonjwa na wanahisi wasile vyakula kila wakati, mwanamke akifikisha muhula wa pili, hamu ya kula huongezeka.
Sababu ya hamu kuongezeka ni, mtoto aliye tumboni anahitaji chakula pia. Unaweza kuona mama aliyekula chakula sahani moja, anaanza kula sahani moja na nusu na baada ya muda si mrefu anahisi njaa tena.
Homoni zilizo mwilini hubadilika na kumfanya mwanamke aliye na mimba kuwa na hamu ya kula kila wakati ili mtoto aweze kupata nguvu na kukua vema.
Kulala mara kwa mara
Wakati mwanamke amekuwa mja mzito, Homoni (progesterone) huongezeka zaidi mwilini. Tulivyonena hapo mbeleni, homoni hii hufanya kazi mwilini kuzembea.
Hii ndio sababu ya wanawake wengi walio na mimba kuhisi usingizi kila wakati. Tukumbuke kuwa, mwana/mtoto anayetengenezwa chupani mwa mamake, anahitaji nguvu zote ili kujistahimili.
Akina mama wanaochukua muda wa kupumzika huwasaidia wanawe kukua kwa njia bora. Pia, afya ya mama huongezeka anapochukua muda wa kulala wakati ana mimba.

Unawezaje kujua kuwa una mimba?
Baada ya kufanya ngono bila kinga, na wakati mwanamke amefikisha umri wa kupata mimba wakati msichana huanza mzunguko wa hedhi  akiwa na dalili zote zilizotajwa hapo awali,  jaribu kwenda na kuhakikisha na daktari ili isiwe ni alama ya chanzo cha ugonjwa fulani na wala si mimba.
Ni muhimu kuhakikisha una mimba wakati unapofikiria u mjamzito. Pia ukisha pata uhakikisho, unaweza kuchukua vipimo bora vya kujitunza wewe na mwanao.
Mwanamke yeyote aliyegundua yuko na mimba anahitajika kutibiwa vyema na wale walio karibu naye. Kila mwanamke anastahili kuoneshwa heshima haswaa wale wanaobeba maisha ndani yao.
Imeaminika mwanamke aliye na furaha kila wakati anapokuwa na mimba huweza kuzaa vizuri na watoto wao pia huwa na furaha.

Tanbihi:Mama mjamzito ahakikishe anapata chakula bora na salama bila kusahau mazoezi mepesi ili uzao wake uwe bora na salamaa..
Wasambazie na wengine waelimike..

No comments:

Post a Comment

Pages