ASILI YA UCHAWI HII HAPA. - waleo blog

Breaking

Sunday 2 February 2020

ASILI YA UCHAWI HII HAPA.


#GHAIBU
Ndani ya makala hii,huenda baadhi ya istilahi zikakukera, tusameeane.
Uchawi (Witchcraft)
 Ni vitu visivyoonekana kwa macho ya kawaida,isipokuwa kwa uchawi wenzake au ucha mungu.’’Kwa maana hii inatufumbua ya kuwa,mtu akikwambia kuwa ni mchawi,basi na yeye ni mchawi.Ima anao ndani ama ameenda kwa mganga(mchawi wa wachawi) kukutazama(kupiga ramli), pia nao ni uchawi haufai kufuatwa na tujiepushe nao maana unaangamiza’’Ucha mungu;ni hali ya kumtaja mungu kila wakati ima ukawa kanisani,msikitini na nyumbani.Kwa kitendo hiki cha kuwa karibu na mungu kwa utulivu;Mungu akitaka anaweza kukuonesha vitendo vya kichawi vinavyofanywa kwako...Uchawi; ni nguvu zinazotumiwa na watu wenye maarifa maalumu yasiyo ya kisayansi katika jamii nyingi duniani, zikiwemo za AfrikaAsiaUlaya n.k., ingawa kuna tofauti nyingi kulingana na mahali au utamaduni.

Lengo lake ni kujaribu bahati,majalibu kwa watu na kujilinda na maadui wengine kimazingara, au kwa ajili ya kujifurahisha, japo wenye imani potofu hulichukulia maanani na kupandikiza chuki kwa ndugu jamaa hata jirani kuwa ni mchawi.
Kwa mujibu wa vitabu vya dini, uwezo na nguvu zote za asili ni za muumba wa mbingu na ardhi na vyote vilivyomo, hivyo yeye anampa mwanadamu uwezo  tofautitofauti kama apendavyo, kwa maana uwezo huo hufanya kazi katika hali ya kubahatisha, yaani ni bahati, hakuna mwenye mamlaka ya kuongoza uwezo huo wa asili ila Mwenyezi Mungu.
Hebu tuutazama Uislamu na historia ya uchawi na walioufundisha.
Baada ya kifo cha Mtume Sulayman bin Daud a.s (mfalme)., Ibilisi alitengeneza uchawi kisha kuuviringa na nyuma yake aliandika kuwa; mzigo huu umetengenezwa na Asif bin Barkhiyyah kwa ajili ya ufalme wa Mtume Suleyman, na kwamba imetolewa kutoka hazina ya ilimu. Na kwa nguvu zake kila jambo linawezekana. Na baada ya hapo aliifukia chini ya kiti cha Mtume Sulayman a.s. Na baadaye aliifukua chini ya kiti hicho na kuidhihirisha mbele ya watu wa zama hizo. Kwa kuyaona hayo, wale waliokuwa wakimpinga mfalme Selemani a.s. walianza kusema kuwa Mtume Suleyman a.s. aliweza kuwatawala kwa uchawi lakini wale waliokuwa waumin walikuwa wakisema kuwa Mtume Sulayman a.s. alikuwa ni mjumbe wa Mungu swt na mwenye imani. Mwenyezi Mungu swt anatuambia kuwa ni shetani ndiye asemaye kuwa Mtume Suleyman a.s. alikuwa ni mchawi. Na jambo hilo ndilo walilolifuata na kuliamini Mayahudi. Lakini Mtume Suleyman a.s. kamwe hakufanya tendo lolote la kukufuru au la ushirikina hivyo kamwe hawezi kuwa mchawi. Wale wanaohalalisha uchawi ni wapingaji kwa sababu Mashetani walikuwa wakifanya uchawi na kuwafundisha watu uchawi na ushirikina.
Baada ya kupita zama za Mtune Nuhu a.s., kulikuja zama moja ambamo wakazi wake walikuwa wakijishughulisha mno na mambo ya uchawi na ushirikina, kwa sababu ya kufuata imani hizo zilizopotofu, kulikuwa kukitendeka matendo maovu kabisa. Hivyo wakazi walikuwa wameupuuzia ujumbe aliokuja nao Nuhu a.s,, na kwa hayo Mungu mtukufu aliwatuma malaika wawili waliokuwa wakiitwa Harut na Marut, ambao walitumwa katika mji uitwao Babul, katika maumbile ya mwanadamu ili waweze kuwazuia wanadamu wasiendelee na uchawi na ushirikina uliokuwa umepindukia kiasi.

Malaika hao walitii amri ya Mungu mtukufu na walimwelezea Mtume wa zama hizo kuwa uwafundishe mambo fulani fulani wakazi wako ili waweze kujiepusha na uchawi na ushirikina huo uliokuwa umewapotosha kabisa. Basi Mtume huyo aliwaambia watu wake kuwa wajifunze mafunzo hayo makhsusi ili waweze kujiepushe na uchawi na kamwe wasiwatendee chochote wenzao. Mungu mtukufu anatuambia kuwa katika mji huo wa Babul kulikuwapo na Mayahudi ambao wao kwa hakika walikuwa wakitenda kinyume na kile walichokuwa wakiambiwa na Mtume huyo, yaani wao badala ya kuutokomeza uchawi, wao ndio wakawa wanauabudu  na wakawa wakifanya uchawi. Malaika wakawaambia sisi tunawafundisheni haya kwa ajili ya kutaka kuwajaribu na kuwajua wale waliona imani ya kurudi kwa  Mungu mtukufu na hivyo kujiepusha na uchawi. Na kutaka kuwatambua wale walioasi na kutumia elimu hii kwa ajili ya kuwadhuru wengine.
Hapo ndipo watu walikuwa wakijifunza uchawi za aina zote mbili yaani watu hao walikuwa wakijifunza uchawi uliokuwa umezuliwa na Shaytani kwa jina la Asif bin Barkhiyyah na elimu waliofundishwa na Mtume Suleyman a.s. kwa ajili ya kujikinga na uchawi wa aina yoyote. Wao walikuwa wakijifunza uchawi hata wa kuwatenganisha mume na mke wake na walikuwa wakiwapatia hasara kubwa sana watu.
Kadiri ya dini mbalimbali watu wote wanaotumia nguvu hizo za asili katika hali isiyoruhusiwa na Mungu, wapo kinyume na Mungu Muumbaji wa mbingu na dunia, hawajui kuwa yeye ndiye mwanzilishi wa nguvu zote za asili ikiwa ni pamoja na wanadamu.
Elimu pia inaweza kusaidia kuondoa imani hizo kwani hata baadhi ya madhehebu ya dini zinachochea kuziamini imani hizo. wasomi wa karne ya 1- 21 na zijazo wanapinga na watapinga  imani hizo haramu ambazo zimesababisha na zinasababisha mateso kwa wazee wasio na hatia hasa vijijini wakishutumiwa kuwa ni wachawi. Tena kumekuwa na mafarakano na chuki katika jamii na familia mbalimbali kwa ajili ya imani ya uchawi; kwa mfano, watu kuuana, kuharibiana mali  kwa kuhisiana uchawi kwa sababu ya watu waliopandikizwa imani za kishirikina.

Serikali ya Tanzania imetumia jitihada zaidi pamoja na kuelimisha wananchi hasa kutokana na suala la imani potofu na tafsiri mbaya ya uchawi ambayo imepelekea watu takribani 5000 kupoteza uhai toka mwaka 1961 kutokana na mateso, kuchomewa nyumba na vibanda katika mikoa ya TaboraKigomaShinyanga na mikoa mingine; ni vilevile katika sehemu mbalimbali za Afrika ya Mashariki na ya Kati. Mwaka 2008 raisi wa Tanzania Jakaya Kikwete alilaani uchawi kama chanzo cha mauaji ya maalbino 25. Imani hizo potofu.

share na wengine wafahamu

No comments:

Post a Comment

Pages