MAGONJWA 16 YATIBIWAYO NA MPERA. - waleo blog

Breaking

Thursday 23 January 2020

MAGONJWA 16 YATIBIWAYO NA MPERA.


#TIBA MBADALA


Kati ya mimea yenye faida kubwa katika mwili wa mwanadamu ni tunda la pera ni moja wapo.Asili ya mti huu ni Amerika na hulimwa sana Amerika ya kusini na kati.
 Majani ya tunda la mpera yakitumiwa vizuri yanaweza kukuletea matokeo ya kushangaza katika nywele hasa kwa watu wenye tatizo la kukatika kwa nywele na mwili kwa ujumla
 Majani ya mpera yana kiwango kikubwa cha Vitamin C, Vitamin A, fiber na potassium.
Wanawake wengi wanaopenda urembo wa nywele wamekuwa wakihangaika na ‘steaming’ za bei mbaya kisa tu kujaza nywele kichwani na kuzifanya zisikatike,
Wasiokuwa na muda wa saluni na wasiokuwa na hela hizi ni habari njema kwao kwamba majani ya mpera ni mazuri kwa kukuza nywele na kuzitibu zile zinazokatika.
Jinsi ya kuyatengeneza kama dawa
 Chukua majani yanayotosha kwenye kiganja chako kisha weka kwenye sufuria yenye lita moja ya maji, chemsha kwa muda wa dakika 15 mpaka 20.
 Baada ya hapo, yaache yapoe kisha paka kwenye nywele zako kuanzia kwenye mzizi wa nywele mpaka mwisho.
 Ukimaliza fanyia masaji nywele zako kama mtu anayepaka mafuta nywele zote.
Baada ya hapo unaweza kuacha kwa muda kama steaming kisha ukaosha.
 Fanya hivi mara kwa mara, walau mara 3 kwa juma, naamini utaona mabadiliko.

        FAIDA   YA  TUNDA  LENYEWE
Mapera ni miongoni mwa matunda yenye kiwango kizuri cha vitamin C pamoja na vitamin A na inaelezwa kuwa kiwango cha vitamin C kinachopatikana ndani ya pera ni mara nne ya kiwango cha vitamin hiyo kinachopatikana kwenye chungwa.
 Pia mapera yamesheheni virutubisho mbalimbali ikiwa ni pamoja na vitamin B2, E na K pamoja na madini ya chuma, ‘copper’, ‘potassium’ na ‘manganese.’
 Kwa mujibu wa utafiti uliowahi kuchapishwa na Jarida la Journal of Human Hypertension mwaka 1993 ulieleza kuwa tunda aina ya pera hupunguza kiwango cha msukumo mkubwa wa damu ndani ya mwili yaani ‘High Blood Pressure’ hii ni kwa sababu ya madini ya potassium na vitamin C ambayo husaidia kuweka sawa msukumo wa damu ndani ya mwili.
1. Utajiri wa Vitamin C:
 Mapera yana utajiri mkubwa wa Vitamin C ambayo ni muhimu sana katika mwili wa mwanadamu.
2. Ni kinga nzuri ya kisukari.
 Ulaji wa watu wengi unawaweka katika hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari lakini matumizi ya mapera yatakupunguzia hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari. Hii ni kwa sababu mapera yana utajiri mkubwa sana wa Fibre.
 Fibre ni muhimu sana katika kupunguza kiasi cha sukari kwenye damu. Vilevile ni muhimu sana katika kuusafisha mfumo wa usagaji.

3. Kuimarisha Uwezo Wa Kuona
 Mapera yana utajiri mkubwa sana wa Vitamin A au Retinol ambayo ni muhimu sana katika kusaidia kuona vizuri.
 Hivyo basi kama ilivyo kwa karoti, mapera yanasaidia sana katika kuongeza na kuimarisha uwezo wa mtu kuona.

4. Kusaidia katika Uzazi
 Mapera yana madini yaitwayo Folate ambayo husaidia katika kurutubisha mayai ya uzazi..
 5. Kurekebisha Kiwango Cha Shinikizo la Damu
 Madini ya Potassium yaliyomo ndani ya mapera yanasaidia katika ku-normalise shinikizo la damu (Blood Pressure)
 Ndizi na mapera vina kiwango cha potassium sawa.

6. Utajiri mkubwa wa Madini Ya Shaba
 Mapera yana madini ya shaba (Trace element copper) ambayo ni mazuri sana katika ku- maintain ufanyaji kazi wa tezi ziitwazo thyroid.
 Tezi za thyroid zisipofanya kazi vizuri zinaweza kusababisha matatizo mengi ya kiafya kwa mwanadamu.

7. Utajiri wa Madini Ya Manganese
 Mapera yana utajiri mkubwa wa madini ya manganese ambayo yanausaidia mwili katika kunyonya ama kupata virutubisho muhimu kutoka kwenye vyakula tunavyo kula.
 Chakula tunachotumia kikitumika vizuri mwilini, tunapata virutubisho vyote muhimu kama vile biotini, vitamin nakadhalika

8. Kuusadia mwili na akili katika kurelax
 Mapera yana utajiri mkubwa wa madini ya magnesium ambayo hufanya kazi ya kuvifanya akili na mwili wa mwanadamu viweze ku relax. Unashauriwa kutumia mapera baada ya kazi nzito. Hii itasaidia katika kuufanya mwili na akili yako kupumzika.

9. Mapera ni muhimu katika afya ya akili ya mwanadamu.
 Vitamin B3, Vitamin B6 ambazo zinapatikana ndani ya tunda la mpera muhimu katika kuimarisha afya ya akili ya mwanadamu.
 Mapera yatasaidia kuufanya ubongo wako u relax.

10. Ni muhimu katika ngozi ya mwanadamu
Vitamin C, viondoa sumu na karotini ambavyo vyote vinapatikana ndani ya tunda la mpera ni muhimu sana katika kuimarisha afya ya ngozi.
 Kama hiyo haitoshi, kokwa la mpera huwa linatumika katika kutengeneza vipodozi na losheni kwa ajili ya matumizi ya mwanadamu.

FAIDA 16 ZA MAJANI YAKE

1. Chai ya majani ya mpera inaponyesha kifua na kikohozi,
1.      Majani ya mpera yaliyosagwa vizuri yanatumika kutibu muwasho uliotokana na mzio (allergy)
2.      Pia majani haya ya mpera yakichemshwa kama chai yanaondoa cholesterol iliyozidi mwilini
3.      Chai ya majani ya mpera inapunguza kiwango cha tatizo la sukari mwilini
4.      Chai ya mpera ni dawa nzuri kwa wenye matatizo ya nguvu za kiume
5.      Pia inatumika kama scrub ya uso chukua majani ya mpera saga kisha tia maji kiasi na inasaidia kuondoa uchafu usoni
 7. Pia majani ya mpera yakichemshwa ni dawa ya kuponyesha tumbo la kuhara
8. Kama umejikata kidogo unaweza kutumia majani ya mpera yaliyoshwa na kusagwa vizuri kwa kupunguza maumivu na kukulinda na maambukizi ya bakteria
9. Majani ya mpera yaliyosagwa vizuri yanatumika kutibu eneo la mwili lililong’atwa na mdudu na kupunguza maumivu
10. Chai ya majani ya mpera inaaminika kuwa ina uwezo wa kutibu tezi dume
11. Kutokana na kuwa na vitamini C kwa wingi majani ya mpera yana uwezo mkubwa wa kutibu chunusi
12. Chai ya majani ya mpera inasaidia kupunguza uzito mwilini na kuzuia uharibifu ndani ya sukari mwilini
13. Majani ya mpera yanajaza nywele na kurefusha nywele kwa watu wenye tatizo la kukatika kwa nywele, unasaga na kuchemsha kisha acha yapoe ndio upake kichwani kutoka chini ya ngozi ya kichwa hadi kwenye ncha ya nywele zako
14. Ukiwa na tatizo la vidonda kwenye ufizi, maumivu ya jino na ufizi tafuna majani ya mpera na utaona maajabu ya majani haya
15. Chukua majani ya mpera saga vizuri mpaka yawe laini kabisa ongeza na maji kidogo kisha tumia kupaka usoni kama scrub inatibu ngozi inayoanza kuzeeka mapema
16. Chai ya mpera inasaidia kwa kutibu mvurugiko wa tumbo.
Pamoja na majani hayo kuwa msaada wa kutibu maradhi mbalimbali , halikadhalika juisi ya mapera nayo husaidia sana kutibu mgolo au bawasiri, figo na hata kuondoa mafuta katika moyo.
Kimsingi mti wa mpera karibu kila sehemu yake ni tiba kwani hata mizizi yake inapochemshwa na kutumia kwa kunywa huenda kuwasaidia wanawake wenye matatizo ya hedhi au wenye matatizo ya kutokwa na maji yenye harufu mbaya sehemu zaoza siri.
Sanjari na hayo, watoto wadogo wenye matatizo ya kutopata choo zaidi ya siku mbili, wakinyweshwa maji ya majani hayo baada ya kuchemshwa huwasaidia kuondokana na shida hiyo, lakini ni vyema kuwasiliana na wataalam wa tiba asili kabla ya kuamua kutumia majani hayo kama tiba kwa mtoto.
 Asante kwa sasa, share zaidi makala hii ili watu wengi zaidi wajifunze.
 
Jumasaidy2328@gmail.com/0712172328

No comments:

Post a Comment

Pages