YAFAHAMU MAAJABU YA MNYAMA SIMBA - waleo blog

Breaking

Monday 16 December 2019

YAFAHAMU MAAJABU YA MNYAMA SIMBA


#UTALII       
   
  Simba ni mnyama wa pili kwa ukubwa katika wanyama jamii ya paka duniani, sio hivyo tu nani wa 1 [kwanza] kwa ukubwa barani Afrika.Wa kwanza ni Puma [Tiger]  na wanyama wengine  jamii ya paka  yaani  Chui, Duma, paka wa dhahabu na paka wa  nyumbani.Simba  wanapatikana katika mbuga zote nchini.Simba wanapenda kuwinda wanyama wakubwa kwa ajili ya chakula, kama vile Nyumbu,Nyati, Punda milia na wengine wakubwa.’’Loooooooh!!!!! niweke angalizo  hata mimi mwandishi na wewe msomaji wa makala hii tukijichanganya kwa Simba huenda tukawa msosi  kwao.Hivyo basi tuwe makini tuingiapo hifadhini kufanya utalii .Lakini pia tuepuke uindaji haramu yaani ujangili,maana ni hatari ukikutana na mnyama kama jamii ya Simba’’.Simba dume  ni mkubwa kuliko Simba jike.Tofauti kati ya  dume na jike ni; Simba dume ana kichwa kikubwa na ni  mwenye nywele nyingi na ndefu shingoni mwake ziitwazo [mane].Pia Simba dume  lina uzito wa kilo 200-250. Simba jike yeye hana kichwa kikubwa wala nywele nyingi na ndefu shingoni mwake.Simba jike yeye ana uzito wa kilo 120—150. ‘’Dah wacha nishangae kidogo na kutafakari maisha ya myama huyu, yaani jike huhimili uzito wa kilo 50—100 za mmewe? Kweli  simba jike  pia ni mvumilivu wa ndoa yake.Wake zetu sasa ungesikia__________..haya bwana ‘’.  Pia  simba jike  ndio mtafutaji chakula{ mwindaji} na dume ndie huwa  mlinzi wa  familia.’’kikwetu kwetu hapa utasikia,, baba Yule mvivu kweli mara anamtesa mkewe mhh! wakati haki sawa kwa wote’’.
          Simba huwa hawali chakula kila siku,yaani simba akiwinda mnyama leo na  wakala wakashiba, basi hukaa na shibe hiyo ndani ya siku tano[5] mpaka saba[7] ndio wale tena.
          
         Fungate(honeymoon)     makubwa kweliii!!! Kumbe simba ndivyo walivyo
’’ha ha haaaaaa
  anapopambana na  dume mwenzie na  kufanikiwa  kumshinda  basi humchukua  Yule jike wa Yule dume aliye mpiga.’’ Eeeehe nini kifuatacho?’’.Simba  jike  ambaye  mumewe amepigwa,  basi  huwa mke rasmi wa Yule dume ambaye ameshinda. Na baada ya hapo huchukua  maamuzi ya kwenda kutafuta   chakula (kuwinda) na anapofanikiwa kupata chakula , basi huja nae Yule mnyama aliye muua na kula nae Yule dume mpya ambaye ndio mmewe.Baada ya kula na kushiba, basi huanza tena kufanya  kile ambacho kinafanyika katika fungate(kujamiiana/tendo la ndoa)..Tendo la ndoa hilo hudumu ndani ya siku tano[5] mpaka saba[7], mpaka palee mimba ya dume mpya itakapopatikana.
o!!’’.Simba dume
           Simba  wakisha jamiiana na kupata ujauzito basi hulea ujauzito huo ndani ya miezi mitatu [3] na huzaa watoto  4-5. Hapa simba huwa ni mkali sana kwa kuwa  huhitaji kuwatunza wanawe wakue kwa salama na amani.
           Simba huishi miaka 20-25 na baada ya hapo ni umauti, kama ilivyo ada kwa viumbe wote..
           Adui mkubwa wa simba ni binadamu na maradhi.

Huyu ni Simba kwa uchache sana hali na tabia zake.
Usisahau  kutufuata (follow)na kutoa maoni  ama ushauri wowote ule katika makala na habari mbali mbali.

 Kwa mambo yote kuhusiana na utalii usisite kututembelea katika:-
malamboaziz14@gmail.com/0717475992/0782080716

1 comment:

Pages