📚 TABIA YA KUGHAIRISHA SEHEMU 2⃣ - waleo blog

Breaking

Monday 3 June 2019

📚 TABIA YA KUGHAIRISHA SEHEMU 2⃣


📚 TABIA YA KUGHAIRISHA SEHEMU 2⃣

MUENDELEZO.
➡ SABABU YA KISAIKOLOJIA KUHUSU KUGHAIRISHA MAMBO.
Katika sehemu iliyopita tuliangalia sababu ya kisayansi kuhusiana na tabia hiyo.
      ➡ utafiti wa kisaikolojia ulibaini watu wengi hupenda kuwaza,kuangalia na kufanya vitu kwa sura ya nje kwasababu ya MAZOEA.
Watu wanaishi maisha yao kwa MAZOEA. Katika kitabu cha sayansi ya tabia kinasema tabia zote nzuri na mbaya ni matokeo ya mazoea ya kurudiarudia mambo.
         Utafiti wa kisaikolojia unaonesha ili uweze kuidhibiti tabia ya kughairisha mambo unatakiwa utambue umeathirika na mazoea yapi yanayopelekea tabia hiyo.
➡Kuna aina au makundi saba (7) ya watu katika tabia ya kughairisha mambo.Hiyo imefafanuliwa katika kitabu kijulikanacho kwa jina la VIZUIZI VYA KUGHAIRISHA ( Ant procrastination).
🌐 Tuangalie aina moja hadi nyingine.
 1⃣ Kundi la watu wanaopenda kufanya vitu bila kujali chochote.
Watu hawa hufanya chochote atakachokiona au kusikia mbele yake kwasababu tu anaamini atapata kitu au kumlipa.Kwa kifupi hili ni kundi la watu wasio na vipaumbele katika maisha yao. Hufanya vitu kwa msukumo tu wa matokeo na sio kufanya vitu kwa kumaanisha,kwasababu hiyo ni rahisi sana kupoteza uvumilivu wanapo kosa au kuchelewa kupata matokeo na kupelekea kughairisha.
2⃣ Kundi au aina ya watu wanaoghairisha kwasababu ya kutojua hatua za kuzifuata katika kazi au jambo husika.Watu hawa hupenda na fufanya vitu lakini hufanya bila kujua na kufuata njia sahihi katika kazi hiyo na kumpelekea kutofikia kiwango kikubwa cha matokeo,hiyo huwaumiza na kupelekea kukata tamaa na hatimaye kughairisha
3⃣ Kundi au aina ya watu wanaoghairi kwasababu ya kusubiri mpaka mambo yote yakae vizuri.Utasikia nikipata fedha kiasi fulani au nikijaliwa nitafanya biashara furani.
4⃣ Kundi au aina ya watu wanaojiona wanamambo mengi kiasi cha kukosa nafasi ya kufanya mambo au kazi nyingine.
Mara nyingi hawa ni wale watu wanaoona au kuzani kila kazi lazima wafanye wenyewe hawafikirii kukabidhi majukumu kwa watu wengine.
5⃣ Watu wanaoona hawana muda wa kufanya mambo kwa sasa na wanaamini watafanya wakipata muda.
6⃣ kundi au aina ya watu wanaoghairisha kwasababu ya kusahau mambo au vitu.
Kusahau kunaweza sababishwa na mambo mengi,kupuuza,kutoona umuhimu,kuhisi kushindwa n.k
7⃣ Kundi au aina ya watu wanaofanya mambo kwa kuangalia watu wengine.
Watu hawa wamegawanyika katika makundi mawili
(I) Wale wanaoepuka lawama.Wanahisi watu wanafuatilia mambo yao hivyo watamuonaje atakapo fanya hiyo kazi.
(II)e Wale wanaopenda wakifanya jambo wasifiwe.
Watu hawa wasiposifiwa huhisi kama kazi au jambo hilo halifai.
✳ Hayo ndio makundi au aina saba za watu katika tabia ya kughairisha mambo.
Katika sehemu ya pili ya somo hili tutaangalia kundi moja baada ya jingine kwa undani na namna ya kujinasua katika hiyo hari inayokuathiri.
✳ Je wewe una angukia katika kundi lipi kati ya hayo saba tuambie.    Itaendelea.............
       By
   Sixbeth Msita kutoka 🇹🇿 MSITA SUCCESS CLINIC🇹🇿
  0692786550

No comments:

Post a Comment

Pages