JE MESS KUITWAA BALLON D'OR? - waleo blog

Breaking

Monday 3 June 2019

JE MESS KUITWAA BALLON D'OR?


 BALLON D'OR


Ronaldo kwa sasa ana mfadhaiko mkubwa baada ya klabu yake mpya,Juventus kutimuliwa ligi ya mabingwa na Ajax katika hatua ya robo fainali.

Labda turudi nyuma hadi 2006,ambapo mshindi wa Tuzo ya Ballon d'Or hakufika hata hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa lakini hata hivyo,Fabio Cannavaro alibeba Kombe la Dunia mwaka huo.jambo hili liliondoa kelele za ushindi huo.Ikumbukwe kuwa mwaka huo Ronaldinho alishinda taji la 'Conferedation CUp' na timu yake ya taifa,Brazil huku taji lingine alilokuwa akilitumaini ni La Liga pekee.

Licha ya kuwa alikuwa na magoli 13,usaidizi(assists) 16 na ufundi mwingi uwanjani,hii haimkufanya ampiku mshindi wa mwaka huo,Cannavaro!

Labda hii inaweza kuwa sawa na mshindi wa Ballon d'Or kuwa K. Mbappe huku taji analoshindania nalo Ligue 1 pekee.

Hata hivyo si mara zote mafanikio ya timu yakampa mchezaji Ballon d'Or.Walikuwepo kina Sneijder na Frank Ribery miaka ya 2010 na 2013,licha ya mafanikio ya timu zao lakini hawakufua dafu.

Kwanini mtu ashinde tuzo hiyo?....Leo hii ni dhahiri kuwa Ronaldo amejiweka mbali na ndoto ya kutwaa Ballon kwa mara ya sita.Wakati mpinzani wake mkubwa (Messi) akijiweka siti ya mbele kuchukua tuzo hiyo.

"Hata kama hatachukua UEFA,lakini bado mesi anastahili kushinda Ballon d'Or". Rivaldo,mwanzoni mwa wiki hii.
"....amekuwa akifunga,akitoa 'asisti',amekuwa mfungaji bora wa La Liga kwa muda mrefu,na sasa anafanya hivyo ligi ya mabingwa,"

Ikumbukwe kuwa,baada ya Ronaldo kutolewa kwenye ligi aipendayo,Messi alikuja juu akiifungia timu yake mabao mawili na kuipeleka nje ya mashindano Manchester United na sasa anaisubiri Liverpool katika nusu fainali.
"Messi ni mchezaji bora wa dunia,na ameonesha hivyo kwenye mchezo wa leo".Jesse Lingard aliongea baada ya mechi.Maneno yake yanatiwa na nguvu na kocha wake,Ole Gunnar ambaye alisema "Niseme tu Messi ni mchezaji bora na leo alikuwa hivyo".

Messi na magoli 45 na usaidizi mara 21 katika michezo 42 msimu huu,rekodi hii inamfanya kuwa bora miongoni mwa wsenzake huko Ulaya.Huenda Messi akimpiku Ronaldo kwa kutwaa Ballon d'Or ya sita,hii inakuja baada ya ronaldo kuondolewa kwenye ligi aliyokuwa anaitegemea miaka ya hivi karibuni.

"Sijaona mchezaji bora kama Messi".Nahodha wa zamani wa Barcelona,Josep Maria aliiambia redio MARCA.

...muda mwingi nilidhani Pele na Di Stefano walikuwa bora,lakini Messi anakaa mbele yao,huyu Muajentina atashinda Ballon d'Or"!

Beki kisiki huko Liverpool na timu ya taifa ya Uholanzi,Van Dijk,anaongoza safu ya ulinzi ya Liverpool,na mwaka huu ataongoza timu yake taifa kwenye UEFA Nations Leaugue ikiwa ni katika cha mwaka mmoja tangu waliposhindwa kufuzu kucheza kombe la dunia nchini Urusi.

Raheem Sterling,anatajwa tajwa kutokana na mchango wake katika klabu yake ya Manchester City ambayo ndiyo mpinzani mkubwa wa Liverpool katika kutwaa taji la ligi kuu Uingereza msimu huu.Hata hivyo kuondelewa kwa klabu yake kwenye ligi ya mabingwa kunamuweka mbali na tuzo hiyo.

Luis Suarez na Allison pia wanawekwa mstari wa mbele,wao ni kama Messi,watakuwa kabiliana na Kombe la Mataifa bara la Amerika(Copa America) mwaka huu.Na Mohamed Salah atakuwa na kibarua cha kuibeba Misri kwenye AFCON,mashindano yatayofanyika nyumbani kwao.

Lakini miongoni mwa washambuliaji wanaodokezwa,Messi anawazidi kwa mambo muhimu katika kunyakua Ballon d'Or,labda kwa Luis Suarez,lakini na yeye ana kazi kubwa ya kumpita mwenza wake,Lionel Messi.

Ronaldo anaweka rekodi ya kushinda Premier league,La Liga na Serie A.Lakini ndoto yake ya kutwaa Ballon d'Or kwa mara ya sita awezi

No comments:

Post a Comment

Pages