KINYONGA NI HATARI KWA BINAADAMU - waleo blog

Breaking

Sunday 23 February 2020

KINYONGA NI HATARI KWA BINAADAMU


#UTALII

Vinyongavigeugeu ni aina za mijusi. Wana miguu kama kasuku, ulimi mrefu na pia wana uwezo wa kugeuka rangi zake. Wanapatikana katika AfrikaMadagaskaHispania na Ureno, Kusini mwa AsiaSri Lanka na hata HawaiiKalifonia na Florida, na pia wanapatikana msituni mwa mvua na jangwani.
Vinyonga wengine huwa na sumu. Kwa mfano, kinyonga wa Namakwa ana sumu kiasi cha kuweza kumpofusha binadamu.
Kinyonga ni kiumbe mwenye sifa ya kuwa na rangi nyingi, kiumbe huyu pamoja kuwa na sumu kali lakini ni mpole na hana matumizi mabaya ya sumu hiyo, ni kiumbe anayeogopwa sana japokuwa si mkorofi, pengine yawezekana ni mkwara wake anaotoa kwa kupanua mdomo  anapohisi hatari au muonekano wake tu.  Mbali na kuwa na macho yanayovutia lakini pia ana sifa ya kutembea taratibu sana, si kwamba hawezi kabisa kuongeza  mwendo/spidi la hasha; hata akiiongeza bado haitaweza fanana na viumbe wengine kama mjusi,hivyo usije fikiri hana wanyonge wake katika mwendo wapo wengi tu hawamfikii mwendo kinyonga, kama jongoo, washawasha na hata konokono.
Duniani kuna aina zaidi ya 100 ya vinyonga. Chakula chake kikuu ni wadudu, kama kumbi kumbi, nzi, na wengineo wa aina hiyo, Madume wa vinyonga ndio huishi miaka mingi zaidi ya 2 na isiyozidi mitano.,Wakati majike huishi muda mfupi sana kwakuwa punde tu wanapozaa hufa.


Sifa pekee za kinyonga.
1. Hubadili rangi kutokana na mazingira
Sababu kuu ya kufanya hivyo ni kujikinga na maadui asionekane kwa urahisi, maana uwezo wake katika mapambano ni mdogo.

2
. Huweza kuelekeza macho yake sehemu tofauti.
Kinyonga ana uwezo; jicho lake moja kutazama vitu vya mbele na jicho lake la pili akatazama nyuma na yote yakifika katika ubongo yakachambuliwa.

3
.Ulimi wake ni mrefu kuliko mwili wake wote.
Hivyo silaha yake kubwa wakati wa mawindo ni ulimi wake ambao huweza kuurusha mbali pindi atafutapo chakula chake.

4
. Kinyonga huwa hazai
Maumbile ya jinsi yake huwa hayawezi kutanuka hivyo namna pekee ya kuwatoa watoto wake tumboni ni tumbo lake likimzidia uzito tuu, hujiachia toka juu na kupasuka ndipo watoto hutoka na mama kufa.

5.
Kinyonga huanza kujitegemea kuanzia sekunde aliyozaliwa.
Na hii ni kutokana na mama yake anapokufa ili azae.
6.
Kinyonga ni kiumbe anayethamini sana usalama.
Na ndio maana hata atembeapo hujiuliza mara mbili kabla ya kushusha mguu wake.
7. Hapendi kuonekana onekana sana
8. Huzaliana sana wakati wa mvua
9. Hupendelea kukaa kwenye miti yenye matunda matunda
10. Sumu yake kubwa ni ugoro, ukimpa hiyo kitu atahangaika sana kabla ya kifo kumpata.’’hili lakini ni la kurithi na lenafanya kazi”
11. Anapopata maumivu hubadilika badilika rangi na hiyo humsaidia kupunguza maumivu.
12. Macho yake huzunguka
13. Pamoja na kubadirika badirika rangi lakini kila kinyonga ana rangi yake kuu.
14. Wapo vinyonga wenye rangi nzuri sana hasa ile kuu.
15. Vinyonga pia hutofautiana kutokana na aina zao, wapo ambao huwa na nundu
kichwani, wapo wenye pembe, wapo wanaovimba mashavu, wapo wenye mapezi kama samaki .

16
.Mikono yake ina chembe chembe za nta akikukamata mpaka aamue yeye kukuacha .


Huyo ndio kinyonga kwa uchache,ukamilifu wake utafuata panapo na uhai.
Shambaza na wengine wamjue ili wasimchezee…

No comments:

Post a Comment

Pages