CHANZO CHA WATU WAFUPI(MBILIKIMO) HIZIHAPA. - waleo blog

Breaking

Sunday 2 February 2020

CHANZO CHA WATU WAFUPI(MBILIKIMO) HIZIHAPA.


#UKWELI ULIVYO

MBILIKIMO/VIOMOLO/VIBURUSHUTI
Yaani watu bila kimo cha chini mno; ni binadamu wa makabila ambayo miili yao ni mifupi kuliko kawaida. Wataalamu wanatumia jina la Kiingereza lenye asili ya Kigiriki Pigmy.
Watu wa aina hiyo wa kwanza kufikiriwa ni wale wa Afrika ya Kati, kama vile WaakaWaefé na Wambuti, pamoja na Watwa wa Rwanda na Burundi. Kumbe kama kipimo kinachotumika ni sm. 155, kuna makabila ya namna hiyo hata AustraliaThailandMalaysiafungu visiwa vya Andamani (India), IndonesiaUfilipinoPapua Guinea mpyaBoliviaBrazil na Asia Kusini-mashariki.

Makabila ya Wabilikimo yanapatikana RwandaBurundiUganda,(anitwa TeusoJamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)(anaitwa Kimbundu), Jamhuri ya Kongo (ROC), Jamhuri ya Afrika ya KatiKamerunGuinea ya IkwetaGabonAngolaBotswanaNamibiaMadagaska Afrika ya kusini (anaitwa Koikoi) na Zambia.
Makabila ni tofauti kati yake, lakini ni tofauti zaidi sana na binadamu wengine. Vipimo vya DNA vinadokeza kwamba wana asili moja, ya zamani sana kati ya miaka 60,000 iliyopita yaani  kuliko aina nyingine zote za watu isipokuwa Wasani.
Mbali na makabila ya mbilikimo, kuna watu katika makundi yoyote ya jamii ambao wanaweza kuwa wafupi kupita kiasi kwa sababu 300 na zaidi tofauti za kiafya. Mtu wa namna hiyo kwa Kiingereza anaitwa dwarf.

Bado watu hawa kwa jamii kubwa inasadikika wanaishi msituni na maisha yao ni ya kijamaa.Hupenda saana  kuwinda yaani ndio maisha yao na uvuvi bila kusahaulika.Kuna wakati ilisemeka kuwa wanakula watu walio tofauti na wao ki kimo…..Ni uzushi tu.Si  maneno ya kweli.

No comments:

Post a Comment

Pages