MAMBO YA MSINGI KUYAJUA ILI UISHI NA WATU VIZURI - waleo blog

waleo blog

    • MAKALA
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MICHEZO
    • MAGAZETI

    Breaking

    Thursday, 21 November 2019

    Home MAKALA MAMBO YA MSINGI KUYAJUA ILI UISHI NA WATU VIZURI

    MAMBO YA MSINGI KUYAJUA ILI UISHI NA WATU VIZURI

    diramTechnologies November 21, 2019 MAKALA,

    #MAISHA

    Nimezipenda hizi nasaha. Naamini na nyinyi wenzangu hamtakosa japo machache ya kujifunza:-

    1. Epuka hasira za ovyo na kila mtu
      Kuwa msikivu kabla ya kukimbilia maamuzi (elewa kuwa ukiwa na hasira huwezi kupata suluhu ya jambo)

      2.Usiwatendee wengine ubaya
     Ipo siku ubaya wako kwa wengine utakurejea kama sio kuwarejea watu wa kizazi chako

    3. Usichukue maamuzi kabla ya kutafiti
    Mtuhumu mtu lakini mpe muda wa kumsikiliza, usimshambulie mtu kwa maneno makali bila kuujua ukweli, ukijua ukweli nafsi inaweza kukusuta.

    4. Mchukulie kila mwanadamu ni mkosaji
    Tambua kuwa hata wewe unawakosea sana wengine na wanakuvumilia. Hivyo usiwe mwepesi wa kuwaadhibu wenzio kwa ubaya

    5.  Usipande mbegu za chuki na ubaya
      Usiadhani itakuacha salama chuki hukua kama mti utambaao, ukiipanda ndani ya jamii yako, haitatoka kwako na inaweza kutafuna kizazi chako ukajutia.

    6. Tambua kuwa yule unayeishi nae ni mwanadamu kama wewe
     Mpe heshima na mwonyeshee upendo hata kama huoni anafanana nawe. Maisha ni duara huenda ulikuwa kama yeye au atakuja kuwa kama wewe baadae.
    7. Usiwe muongeaji ovyo ovyo na usiye na subira.
     Kuongea sana kunapoteza busara.

    8. Jiepushe na maisha ya kusukumwa na wengine
     Yaani kufanya jambo usilojua manufaa yake. Jifunze kujitegemea kiakili. Sio kila unayemdhania rafiki moyoni mwake yupo pamoja nawe, na ukashirikiana nae, wengi wa marafiki zetu hututumia sana kuliko tunavyoweza kuwatumia wao.

    9. Usipende sana kugombana na watu kwa njia ya maongezi yanayodumu kama vile
     Ujumbe wa maandishi, mawasiliano ya simu au ujumbe wa maneno (SMS). Kumbuka kuwa maneno yanaishi kuliko ugomvi au uadui, ipo siku yatakurudi na utajiona mpumbavu na kukosa pa kujificha. Jifunze kusubiri
    .
    10.Usifumbue mdomo wako kutamka ubaya au kunyanyua kidole chako kuandika ubaya juu ya mwenzio bila kujiuliza mara mbili moyoni mwako hatima ya unachokitoa kwa mwingine.

    10. Jishushe na jifunze kusikiliza wengine
     Wakati wa mazungumzo ili uweze kujifunza kabla ya kukurupuka kujibu, usikivu ni kipimo cha busara, mtu anayekurupuka kujibu jibu kila anachosikia hawezi kuwa kiongozi, Mume au Mke mwema kwani mara nyingi atapotoka tu

    11. Usitunze hasira nyingi moyoni kwani hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu. Jitahidi pia kuepuka kuwa na hasira mara kwa mara na zisizo na maana. Elewa kuwa hasira zisizo maana hukupunguzia maisha na kukupa maumivu wewe mwenyewe kuliko yule uliyemfanyia hasira, utakufa kwa magonjwa kabla ya wakati ufaao

    12. Thamani yako inategenezwa na watu wengine,
      Wewe kama ni mtoto, mheshimu sana mzazi wako na kama umeoa au kuolewa, heshimu wazazi na familia ya mke au mumeo kwa kuwa bila wao, usingekuwa hivyo ulivyo leo unajivunia ndoa njema, kwa kuwa yupo mtu alimzaa huyo mwenzio. Mheshimu kwa lolote liwe jema au baya, utalipwa kwa wakati ufaao

    13. Usijibizane na mtu usiyemjua au ambaye hawezi kukupunguzia kitu katika maisha yako. Tambua kuwa unapunguza sehemu kubwa ya maisha yako kwa kutafuta magomvi na mtu wa mbali nawe.

    14. Kumbuka asili yako
     kumbuka upo hapo kwa kuwa kuna mahali ulitoka, maisha yanabadilika, usidharau pale ulipokuwa zamani kwa kuwa ndipo palipokufanya leo uwe hapo.

    15. Subiri, sikiliza, elekeza, vumilia
     Elewa sio kila mtu ana uelewa kama wako. Jitahidi kuwa mvumilivu katika kila jambo, usiinuke kuwafokea au kuwakaripia wengine kwa jambo ambalo pengine nao wanahitaji muda kueleweshwa ili walifanye vyema. Kumbuka sana, kuna wakati nawe ulikuwa huelewi kabisa lakini wapo wenzio walikuvumilia, wakakuelekeza njia njema, kufokea wengine mara kwa mara sio njia njema ya kuwafundisha bali ni kuwaweka mbali nawe.

    #SHARE,LIKE,COMMENT  AND FOLLOW US



    Tags # MAKALA
    Share This
    Author Image

    About diramTechnologies

    MAKALA
    By diramTechnologies at November 21, 2019
    Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
    Labels: MAKALA

    No comments:

    Post a Comment

    Newer Post Older Post Home
    Subscribe to: Post Comments (Atom)

    Author Details

    Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.

    Follow us on Social Media

    • facebook count=3.5k;
      Followers
    • youtube count=2.8k;
      Followers
    • instagram count=849;
      Followers

    Followers

    • Home
    • about
    • contact
    Powered by Blogger.

    Recent

    Popular

    • MAJUKUMU MUHIMU YA DIWANI.
      MAJUKUMU MUHIMU YA DIWANI.
      #UTAWALA Diwani  nchini  Tanzania   ni mwakilishi wa wananchi wa  kata  yake, pia ni mwakilishi wa wananchi katika vikao vya bara...
    •   JE!?  WAMJUA MUMEO?
      JE!? WAMJUA MUMEO?
        Leo nimemua kufanya hivi ili niwe msaada kwa wanawake hasa wale ambao wamefikia hatua ya kuingia kwenye ndoa lakini bado wanashindwa kuta...
    • CHAKULA CHA UBONGO
      CHAKULA CHA UBONGO
       #Kikokotoo MAHITAJIA YA   AKILI DOKEZO: #Akili ni nini? Ni uwezo   alionao binadamu,mnyama na wadudu, ambamo ndanimwe ndio matokeo mam...
    • MAMBO KUMI YATAKAYOKUWEZESHA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI
      MAMBO KUMI YATAKAYOKUWEZESHA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI
       #MAHUSIANO kama huwezi kumfikisha mwanamke kileleni basi unausika katika hili somo!!!!…Wengi wakitaka kujua ni namna gani ya kumf...
    • MAGUFULI AONYESHA ALIVYOGUSWA NA MSIBA WA MKAPA
      MAGUFULI AONYESHA ALIVYOGUSWA NA MSIBA WA MKAPA

    Comments

    Pages

    • Home

    Contact Form

    Name

    Email *

    Message *

    Crafted with by Templatesyard | Distributed by Blogspot