MBINU ZA KUEPUKA KUMBEMENDA MTOTO - waleo blog

Breaking

Sunday 23 February 2020

MBINU ZA KUEPUKA KUMBEMENDA MTOTO



#AFYA

Kubemenda ni lugha inayotumiwa na watu wengi kwa maana ya kuwa “mtoto ameharibiwa afya yake sababu ya wazazi wake” mara nyingi taswira hii ya kudhoofika kwa mtoto huendana na matazamio ya kwamba mzazi mmoja (mke au mume) ametoka nje ya ndoa na kutembea na mtu tofauti au mama anayenyonyesha       na kubeba ujauzito mwingine.Kwa kawaida mama mjamzito baada ya kujifungua huchukua muda upatao kati ya miezi mitatu hadi nane kurudia kwenye mzunguko wake wa hedhi (siku zake) bila kujali amepasuliwa au amejifungua kawaida,muda huo ambao hapati siku zake ni vigumu kupata ujauzito mwingine hata kama akikutana na mume.Lakini baada ya kuanza kuziona siku zake ni wazi kuwa uwezekano wa kukutana na mume na kupata ujauzito ni mkubwa sana.
Miongozo ya dini nyingi huelekeza muda wa mume kuweza kukutana na mke wake baada ya kujifungua,na haikupangii wewe ni lini na muda gani utafanya hivyo au ni namna gani utajikinga na ujauzito usiotarajia maana hii huwa ni baraka za mungu kukujalia uzazi.Kwa upande wa tamaduni za jamii zetu ni kuwa mwanamke baada ya kujifungua huweza kuacha kushiriki shughuli za ndoa (tendo la ndoa) akiwa pamoja na mwenza wake (mume) au hata kutengana kabisa na mume wake kwa kipindi fulani kwa ajili ya kulea mtoto aliye zaliwa.
               Kwanini mtoto adhohofike kiafya.
Kuachishwa kunyonya mapema kabla ya mwili wa mtoto haujazoea kutegemea vyakula kujijenga kiafya,hii hupelekea uwezo wa kukabiliana na magonjwa ni mdogo hivyo kuugua mara kwa mara na kupelekea kuzorota kiafya.Hatua hii mara nyingi huchukuliwa kutokana na kubeba ujauzito mwingine kabla ya mtoto aliyetangulia hajamaliza kunyonya.lakini hilo siyo tatizo kwani hakuna uhusiano wowote ambao unaweza kumdhuru mtoto akinyonya maziwa ya mama yake mjamzito.Kumwachisha kunyonya ndio tatizo linalodhoofisha mtoto na siyo mimba aliyobeba mama.
Uchafu wa wazazi (mke na mume)  kutozingatia mazingira na wakati mzuri wa kukaa faragha wakati mtoto akiwa mbali nao.Tunaposema uchafu wa wazazi ni kwamba wazazi  wanashiriki tendo la ndoa na lakini bila kujali kuoga kabla ya kunyonyesha au kumshika mtoto.Faragha kunakuwa na mipapaso,mihemko,kuingiliana kimwili,kulambana,kunyonyana au kuchezeana maeneo mbalimbali ambayo hurudiwa mara kwa mara hivyo huweza kusafirisha uchafu wa sehemu za siri (baada ya kuingiliana kimwili)kuja hadi kwenye mikono,matiti  n.k  kwa namna hii mtoto akinyonyeshwa kabla ya kujisafisha basi atakuwa anakula uchafu na matokeo yake kuharisha na mengineyo.muhimu kuoga kabla ya kunyonyesha na tafuta muda wa kukaa faragha mtoto akiwa amelala au yupo maeneo ambayo huweza kukaa muda mrefu bila kulilia kunyonya.


Miiko na tamaduni mbaya zinazokandamiza upatikanaji wa chakula bora kwa mtoto hasa akiwa bado mdogo,kipindi cha utoto kunahitajika chakula chenye  virutubishi vingi ili kukuza  afya ya mtoto.
Magonjwa ya utapiamlo na mazingira machafu ya kuandalia chakula, hivyo vimelea vya magonjwa huweza kumshambulia mtoto kwa urahisi kutokana na kwamba kinga zake za mwili ni ndogo sana ukilinganisha na kinga za mtu mzima.
Tujitahidi usafi kina baba na kina mama ili motto awe na afya bora.
Share na wengine waelimike na wakumbuke.

No comments:

Post a Comment

Pages